2015-01-24 12:02:02

Jielekezeni katika kudumisha amani!


Wakimbizi na wahamiaji wanaoishi na kuhudumiwa kwenye kambi za wakimbizi nchini Kenya wanahamasishwa kuhakikisha kwamba, wanaishi kwa amani na utulivu na kuachana tabia ya chokochoko na uvunjaji wa sheria; mambo ambayo yamepelekea watu kadhaa kupoteza maisha kwa siku za hivi karibuni.

Hii ni changamoto ambayo imetolewa hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya Siku ya wakimbizi na wahamiaji duniani na Askofu Virgilio Pante, Mwenyekiti wa Tume ya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya kwa ajili ya wahamiaji, wakimbizi na mabaharia. Anasema, kunakosekana mchakato wa upatanisho katika kambi za wakimbizi na wahamiaji, sanjari na kuendeleza misingi ya haki na amani.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa siku ya wakimbizi na wahamiaji anawataka waamini na watu wote wenye mapenzi mema kujenga na kudumisha misingi ya haki, amani, udugu na mshikamano, sanjari na kukomesha mambo yanayosababisha vita, chuki na kinzani.







All the contents on this site are copyrighted ©.