Baba Mtakatifu Francisko akiwa katika hija yake ya kitume Barani Asia, amemtumia salam
za matashi mema, Bwana Giorgio Napilitano aliyekuwa Rais wa Italia baada ya kung'atuka
kutoka madarakani siku ya Jumatano tarehe 14 Januari 2015. Baba Mtakatifu anampongeza
Rais mstaafu Napolitano kwa huduma makini aliyoitoa kwa wananchi wa Italia bila ya
kujibakiza kwa kuonesha uaminifu na uadilifu, kwa ajili ya mafao ya wengi.
Baba
Mtakatifu anampongeza Rais mstaafu Napolitano kwa hekima na busara katika kukuza na
kudumisha mshikamano, umoja wa kitaifa, amani na utulivu mintarafu Umoja wa Ulaya,
hata kama Italia imeguswa kwa namna ya pekee na matatizo pamoja na changamoto nyingi.
Baba Mtakatifu Francisko anahitimisha ujumbe wake kwa kumwahidia Rais mstaafu Napolitano
neema na baraka na kwamba, ataendelea kumkumbuka katika sala zake.
Na Padre
Richard A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.