Rais Napolitano wa Italia ang'atuka kutoka madarakani!
Bwana Giorgio Napolitano mwenye umri wa miaka 89 baada ya kuiongoza Italia kwa kipindi
cha miaka tisa, Jumatano tarehe 14 Januari 2015 amewasilisha Bungeni barua yake ya
kung'atuka kutoka madarakani na hivyo kuacha nafasi kwa Waziri mkuu wa Italia Bwana
Matteo Renzi kuanzisha mchakato wa kumpata Rais mpya wa Italia. Wananchi wengi wa
Italia wanaoishi mjini Roma walimiminika kwenye Ikulu ya Italia, kumwaga Rais Napolitano
ambaye wengi wanamsifia kwamba, amejitahidi kuiongoza nchi kwa moyo wa uzalendo na
uadilifu mkubwa!
Tangu leo, Bwana Napolitano si kiongozi tena wa Italia na
amehamia kwenye makazi yake binafsi. Anakumbukwa sana na wananchi wa Italia kwa kipaji
cha akili, uaminifu na kwamba, alikuwa ni mtu huru aliyekubalika na wengi katika shida
na magumu ambayo Italia imepitia katika historia na maisha yake.
Bwana Napolitano
alikuwa ni mkweli na mtu wazi kwa maneno na matendo yake kamwe hakupenda "longolongo
za kisiasa".