2015-01-12 11:14:18

Uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na Vatican


Mheshimiwa Philip S. Marmo, Balozi wa Tanzania mjini Vatican katika mahojiano maalum na Radio Vatican anapembua kwa kina na mapana mafanikio yaliyokwisja patikana nchini Tanzania katika medani mbali mbali za maisha. Anazungumzia pia mgogoro ulioibuliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutaka kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislam, OCIC na mchakato wa Muswada wa Katiba inayopendekezwa, ili kupata ufumbuzi wa masuala kadhaa kwa Zanzibar. RealAudioMP3

Kwa namna ya pekee kabisa, Balozi Marmo anajadili umuhimu wa Tanzania kuwa na mahusiano ya Kidiplomasia na Vatican, au kwa kitaalam "Holy See" ambayo kwa sasa iko chini ya uongozi wa Baba Mtakatifu Francisko, kwa kutambua kwamba, hii ni Jumuiya kubwa ya waamini ambayo ina mchango mkubwa katika sera na mikakati ya kimataifa na kwamba, mchango wake unathaminiwa sana na Jumuiya ya Kimataifa kama iliuvyojitokeza hivi karibuni kwa suluhisha mgogoro wa kidiplomasia kati ya Marekani na Cuba.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.