Papa abatiza watoto 33: wazazi lisheni watoto pia na Neno la Mungu
Jumapili kwa ajili ya maadhimisho ya Siku Kuu ya Ubatizo wa Bwana, ikiwa pia ni kufunga
kipindi cha Siku Kuu ya Noeli, Baba Mtakatifu Francisco ameadhimisha Ibada ya Misa
katika Kanisa dogo la Sistine la mjini Vatican ,na ambamo pia amebatiza watoto 33
wa wafanyakazi wa Vatican. Watoto hao, wakiwa wanaume 12 na wasichana 21.
Katika
mahubiri yake, Papa amewataka wazazi na wasimamizi, kuelea watoto katika mwanga
wa Neno la Mungu. Na pia akatoa maombi kwa ajili ya akina mama wengi wasiokuwa na
uwezo wa kulisha watoto wao, waweze kupata lishe kwa watoto wao.
Akitoa
msisitizo kwa upande wa kiroho amesema kuwa ,ubatizo ni kuwekeza katika mwili wa Kanisa,
ambao ni taifa la Mungu linalo tembea katika njia Takatifu. Na akakumbusha kwamba,
haiwezekani kuwa Mkristo, nje ya kanisa. Na kwamba, Mwanga wa mshumaa unaowashwa kutoka
Mshumaa wa fumbo la Pasaka, ishara ya Kristo Mfufuka, aliye hai kati yetu, hurithishwa
mkono kwa mkono, kizazi hadi kizazi. Papa alirudia kuutaja urithi huu kwa mama, baba,
wasimamizi wote wake kwa waume , kwamba , imani ya Kanisa ni watu wanaotembea katika
njia ya imani, wakiirithisha imani yao kupitia ubatizo kwa watoto wao.
Papa
aliendelea kuzungumzia juu ya imani ya kanisa akiangalisha pia katika imani ya Maria,
Mama yetu, imani ya Mtakatifu Joseph, Mtakatifu Petro , Mtakatifu Andrea, Mtakatifu
Yohana, imani ya Mitume na Mashahidi, ambayo inajidhihirisha kwa waamini kwa njia
ya ubatizo. Papa amelitaja hili kuwa ni jambo jema, linaloonyesha mwanga wa Kanisa,
ambao ni Mwili wa Kristo, watu wa Mungu , walio katika hija wakati wote na mahali
popote, wakifundisha watoto wao kwamba, hawawezi kuurithi Ukristo wa wazazi bila ya
ubatizo. Na hakuna anayeweza kuwa Mkristo nje ya Kanisa, na haiwezekani kuwa mfuasi
wa Yesu Kristo bila Kanisa, kwa sababu Kanisa ni mama anayetufanya kukua katika upendo
kwa ajili ya Yesu Kristo.
Na hivyo Papa aliwahimiza watu wazima Wakristo
, hasa wazazi, wasimamizi, babu na bibi na ndugu wengine, kuwa mstari wa mbele kulisha
Neno la Mungu, Injili ya Yesu, "chakula kikuu, cha familia, kinachoweza kukua na kuzaa
matunda mazuri katika maisha, kama ilivyo mvua na theluji inyesha juu nchi, huiwezesha
nchi kuzaa matunda. Neno la Mungu ni chakula bora, ambacho hutolewa na Mungu, Baba
Mwema, na Mama mwema, mwenye kuwapa watoto wake, kilicho kizuri.
Papa amemshukuru
Bwana kwa ajili ya zawadi ya maziwa ya mama na kuomba kwa ajili ya akina mama wengi,
ambao kwa bahati mbaya, wameshindwa kuwa na chakula hiki kwa watoto wao. Papa ameomba
uwepo wa uwezekano wa kuwasaidia akina mama hawa. Na akakumbusha kama yalivyo maziwa
kwa mwili, Kiroho ndivyo ilivyo Neno la Mungu. Neno la Mungu hufanya imani kukua.
Papa
ametoa wito kwa wazazi na wasimamizi na watu wazima ndani ya familia, wawe chemichemi
ya maombi. Kumwomba Baba kwa ajili ya mahitaji ya familia na pia Roho Mtakatifu,
daima awe mwalimu mwenye kuonyesha jinsi ya kuibeba familia , ili watoto waweze kukua
na utambuzi wa uwepo wa nafsi ya tatu ya Utatu Mtakatifu, Roho mwenye kuongoza na
kuvuvia kila siku yale tunayopaswa kufanya katika maisha yetu kama waamini. Papa amesali
ili Roho Mtakatifu, aijaze mioyo ya waamini neema zake na kuwasha ndani yao moto
wa upendo wa Mungu.