Askofu mkuu Eugene Martin Nugent, ateuliwa kuwa Balozi Mpya wa Vatican nchini Haiti!
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu mkuu Eugene Martin Nugent, kuwa Balozi mpya
wa Vatican nchini Haiti. Kabla ya uteuzi huu, Askofu mkuu Nugent alikuwa ni Balozi
wa Vatican nchini Madagascar, Mauritius, Seychelles na Visiwa vya Comoro. Askofu mkuu
Nugent alikuwa pia ni mwakilishi wa kitume wa Visiwa vya Riunione.
Uteuzi huu
umefanywa na Baba Mtakatifu Francisko wakati Kanisa la kiulimwengu linafanya tathmini
ya kina kuhusiana mchakato wa ujenzi wa Haiti mpya baada ya kukumbwa na tetemeko la
ardhi yapata miaka mitano iliyopita. Wakati wote Kanisa limeonesha upendo na mshikamano
kwa wananchi wa Haiti kwa njia ya misaada ya hali na mali iliyokuwa inasimamiwa na
Baraza la Kipapa linaloratibu misaada ya Kanisa Katoliki, Cor Unum.