2015-01-09 14:45:37

Ziara ya Kitume ya Papa Francisco Sri Lanka na Ufilipino


Baba Mtakatifu Francisco, wiki ijayo, atakuwa na ziara ya kitume kwa muda wa wiki moja, kutembelea mataifa mawili, Sri Lanka na Ufilipini, tangu Jumatatu hadi Jumapili, 12-19 Januari 2015. Kwa mujibu wa ratiba Papa ataianza safari Jumatatu tokea uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Fiumicino Roma hadi Colombo, Mji Mkuu wa Sri Lanka , mwendo wa saa 9 na dakika 40 hewani, akipita katika anga za Italia, Albania, Ugriki Uturuki, Irani, Shirikisho la nchi za Kiarabu, Oman, India na hatimaye Sri Lanka. Kutokana na tofauti za saa, ndege ya Papa itatua katika uwanja wa ndege wa Colombo Siku ya Jumanne.
Katibu wa Vatican , Kardinali Parolin, katika mahojiano na vyombo vya habari juu ya ziara hii ya Papa , amesema kuwa Papa aìinalenga katika mambo mawili muhimu kwa ajili ya utume wa Kanisa barani Asia, kwanza ni kuhimiza matendo ya hisani katika uwanja wa afya na elimu na pili, ni umuhimu wa kukazia mazungumzo kati ya dini kama chombo muhimu kwa ajili ya amani katika dunia ya leo na hivyo unakuwa ni wajibu kwa dini zote.

Kardinali Parolin, alieleza hilo hasa akilenga kujibu swali lililoulizwa, iwapo Papa Francisko anarudi Asia na ujumbe mpya, katika mtazamo kwamba, imepita muda wa miezi mitano tu tangu alipofanya ziara Korea, ambako katika mazungumzo yake alikazia Kanisa kujikita katika majadiliano kati ya dini.

Kardinali aliendelea kufafanua kwamba, utume wa Kanisa, iwe ufilipino , au Sri Lanka na duniani kote: ni kutangaza Injili, kutangaza habari njema ya Yesu ambaye ni chanzo cha maisha na matumaini ya watu wote. Utume unaofanywa na Kanisa kwa kuzingatia bila shaka, mazingira linamoishi na kufanya kazi. Ni mazingira tofauti tofauti kutokana na kwamba kanisa huundwa jamii mahalia bila kujali mchanganyiko wa jamii kikabila, kitamaduni na dini. Na bara la Asia ni mbeleko ya dini kuu za ulimwengu. Na kwa kuzingatia ukweli kwamba kanisa lina wafuasi wachache, ni kundi dogo, lakini katikati ya ukweli wake ni kundi kubwa katiak maana ya utendaji wake. Na hivyo, bila shaka Papa atatoa ujumbe wake, kulingana na sifa hizo.

Kardinali anasema Papa anaifanya ziara hii, kama hatua ya kuwatia shime Wakristo wa Asia pamoja na uchache wao, kuona wana umuhimu mkubwa katika ufanikishaji wa nyanja mbalimbali za maendeleo ya binadamu, katika vyote kihali na kiroho pia hasa kupitia misaada katika uwanja wa afya na elimu, ambavyo, tayari vinafurahiwa na kupokelewa kwa shukrani kubwa na watu wote na serikali za nchi mbalimbali.

Kwa upande mwingine , Papa analenga kuhimiza zaidi mazungumzo kati ya dini , kwa ajili ya kukuza na kuimarisha zaidi na zaidi, watu kukutana kwa heshima, kukubalika na kuheshimiana, kama alivyoeleza katika waraka wake wa kitume wa Injili ya Furaha, kwamba, mazungumzo kati ya dini, ni muhimu kwa ajili ya amani, katika dunia ya leo na hivyo, unakuwa ni wajibu wa dini zote. Hoja hizi zitakuwa kitovu, cha hotuba za Papa , katika ziara hii.

Kati ya matukio muhimu yatakayofanywa na Papa Francisko katika ziara hii, ni Siku ya Jumanne , atakutana na kuzungumza na wawakilishi wa dini mbalimbali katika kituo cha Congress cha mjini Colombo. Jumatano ataongoza Ibada ya Misa kwa nia ya kumtaja Mtakatifu, Padre mahalia , Ibada itakayo fanyika katika uwanja wa Gale Face Green mjini Colombo. Na jioni ataongoza Ibada ya Rosari katika Madhabahu ya Madhu.

Alhamisi, Papa atasafiri hadi Manila Ufilipino, ambako Siku ya Ijumaa , ataongoza Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la Mjini Manila,Ibada itakayohudhuiwa na Mapadre na Watawa, na baada ye jioni kukutana na familia katika ukumbi mkuwa wa Manila. Jumamosi Papa ataongoza Ibada ya Misa katika uwanja wa ndege wa Tacloban , na baadaye jioni kukutana na Mapadre, Watawa, Wasemnaristi na familia za kafara wa kibunga kaiak Kanisa Kuu la Palo. Jumapili ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara , asubuhi atakuwana na vijana na jioni ataongoza Ibada ya misa katika uwanja wa Rizal wa mjini Manila.

Askofu Joseph Ponniah wa Jimbo la Batticaloa, Mashariki mwa Sri Lanka, naye katika mahojiano anasema, Waamini Wakatoliki, wamejawa na furaha isiyo kifani , kwa kuwa na Papa kwa muda wa siku tatu kisiwani humu kutoka Januari 13-15. Na wengi wana hamu kubwa ya kusikia ujumbe wa matumaini na maridhiano kutoka kwa Papa, kwa sababu wengi wana majeraha ya siku muda mrefu, kutoka mbio za vita vya wenyewe kwa wenyewe, taifa bado kuponywa hasa na majeraha yaliyoachwa na wanamgambo wa Tamil.
Askofu ametajakti ya tukio la kuwasisimua kiroho , ni ibada itakayoongozwa na Papa kwa ajiliya mkutaja kuwa mwenye Heri, Joseph Vaz, aliyeishi karne ya 17, Padre kutoka India ambaye alifanya kazi kubwa, katika kuijenga jamii Katoliki Sri Laka baada ya miaka mingi ya madhulumu na mateso. Askofu Ponniah alionyesha furaha kubwa kwa mmoja wao kutajwa katika daraja hili la utakatifu , akismea Wasyri Lanka wanamatumaini ya kusikia kutoka kwa Papa ujumbe wa amani na maridhiano, neno wanalotamani kwa muda mrefu kulisikia baada ya miongo mingi ya vita vya kiraia na mateso mengi yaliyo fanywa na vita hiyo.
Pamoja na matumaini hayo, Askofu Ponniah pia alionyesha kuwa na wasiwasi wa hali itakavyokuwa , baada ya matokeo ya uchaguzi wa rais, kutangazwa katika uchaguzi unaofanyika siku chache kabla ya Papa kutembelea taifa hilo. Baadhi wanahofu matokeo yanaweza kuleta mtafaruku , lakini wengi wanaimani kwamba, kwa vyovyote itakavyokuwa katika matokeo ya uchaguzi huo, amani na utulivu vitaendelea kutawala.







All the contents on this site are copyrighted ©.