Kila mwaka ifikapo tarehe 9 Januari, Wakristo nchini Ufilippini wanafanya maandamano
makubwa ya Njia ya Msalaba na maandamano ya Mwaka 2015 yanajikita katika huruma na
upendo unaofumbatwa katika maisha na utume wa Kanisa, kielelezo cha kauli mbiu inayoongoza
hija ya kichungaji ya Baba Mtakatifu Francisko nchini Ufilippini. Hili ni tukio ambalo
linawakusanya mamillioni ya waamini kutoka sehemu mbali mbali za Ufilippini ili kushiriki,
baadhi yao wakiwa na imani kwamba, wanaweza kutendewa miujiza katika maisha yao!
Mapokeo
yanaonesha kwamba, Maandamano ya Njia ya Msalaba, tukio la pekee kitaifa yanapata
chimbuko lake kunako karne ya kumi na saba, kutoka Barani Asia. Yesu anayebebeshwa
Msalaba mzito ni Ibada ambayo ilianzishwa na kunako mwaka 1606 na Padre mmoja wa Shirika
la Waagostiani, kutoka Mexico, wakati huo, Ufilippini ilikuwa chini ya utawala wa
Wahispania. Meli iliyokuwa imebeba Sanamu hii, iliungua moto kabla ya kutua nanga
banadarini, lakini Sanamu ya Yesu Msalabani, ikasalimika kwa muujiza.
Kanisa
Katoliki kwa kuthamini mapokeo na imani ya wananchi wa Ufilippini lilitoa kibali na
kwamba, waamini wanaoshiriki katika tukio hili, kwa imani pamoja na kutimiza masharti
yaliyowekwa na Kanisa, wanaweza kupata rehema kamili! Takwimu zinaonesha kwamba, maandamano
haya ya Njia ya Msalaba kwa mwaka 2014, zaidi ya waamini millioni kumi!