Epifania ni sikukuu ya mwanga na mwanga huo ni Yesu Kristu, mwanga unaoangaza. Mwangaza
huo umewaangaza watu wote na unaendelea kuangaza. Ni sikuu ya mafumbo ya utoto wa
Yesu (Rej. KKK 528. Mamajusi ni watu wenye busara wa mashariki ambapo baada ya kuiona
nyota na kwamba bwana amezaliwa, walienda Yerusalemu kumwabudu. Zawadi walizochukua
zilipatikana huko kwao – Yer 6,20. mababa wa kanisa waliona kuwa dhahabu ni mfano
wa ufalme wa kristo, uvumba ulionya umungu wake na manemane ikionya mateso yake. Mamajusi
walimsujudia kristo na ndivyo walivyotumia maneno ya Mungu juu ya Masiya kwamba mataifa
watamwabudu Mungu wa Israeli Hes 24,17.
Ni mwanga kwa watu wote wanaomwendea
Mungu wakiongozwa na imani ya huyo Mungu mwenyewe. Katika Isaya 60:1-6 tunapata habari
juu ya utukufu wa Bwana unaong’aa Yerusalemu (ambao neno wa Mungu utatokea) mahali
ambapo patakuwa ni makutano ya watu wote ili kumtukuza Mungu na kumtolea ubani na
manemane. Katika barua kwa Waefeso 3,2-3,5-6 tunaona kuwa kwa Waebrania walioteuliwa
kwanza na kwa wapagani waliokuja baadaye wote wameitwa katika imani moja kumfuata
kristo na kugawana urithi wa milele pamoja naye. Wokovu wa Mungu ni kwa ajili ya ulimwengu
mzima.
Katika Injili Mt 2,1-12 kutokujali na ujinga wa walimu na wakuu wa
sheria, hofu na wasiwasi wa Herode imekuwa maangamizi kwao. Jibu sahihi la mamajusi
tumeona nyota yake mashariki na tumekuja kumwabudi limekuwa wokovu wao. Wanatoka mbali
na wanapata wokovu ila walio karibu hawatambui kuwa mwokozi amezaliwa.
Maana
nyingine ya Epifania ni kujionyesha au kujifunua. Kwa maana hiyo ya kigiriki katika
dini yao ilikuwa ni desturi kwa mmoja wa miungu kumtokea mmoja wao. Katika maandiko
matakatifu neno hilo halipo bila shaka ni kuepa kuoanishwa na neno hili la kipagani.
Tukisoma tu 1 Mak 1,10 tunaona helenistick king antioochus Epiphanes anayejifananisha
na Mungu anayejionyesha.
Kiyunani Epifania twaona kuwa maneno hayo yaelekezwa
kwa Yesu na kazi yake ya wokovu mpaka siku mwisho. 2 Tim 1:10- na sasa inadhihirishwa
yaani neema ya Mungu kwa kufunuliwa kwake mwokozi wetu yesu kristo Yesu aliyebatili
mauti na kuufunua uzima wa kutoharibika, kwa ile injili. Tito 2,11 maana neema ya
Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunguliwa Tito 3,4 lakini wema wake mwokozi wetu
Mungu na upendo wake kwa wanadamu ulipofunuliwa alituokoa.
Katika Kanisa jina
hili Epifania limeonekana karne ya tatu likitumiwa kwa Yesu hivyo hatari ya kuhusishwa
na upagani ikaisha kwa kweli Yesu ndiyo ufunuao wa Mungu. Kanisa la Mashariki likawa
la kwanza kusherehekea sikuku ya tokeo la Bwana likiunganisha na ubatizo wa Yesu pale
Mto Yordani. Itakumbukwa kuwa katika tukio hilo sauti toka mbinguni ilisikika ikasema
huyu ndiye Mwanangu mpendwa wangu niliyependezwa naye msikilizeni yeye Mk 1:11 Mungu
kwa mara ya kwanza anajifunua kuwa yeye ni nani kwa njia ya Yesu Kristo mwanaye. Kanisa
la Magharibi kwenye karne ya nne likahusisha hija ya mamajusi na toleo la Bwana jinsi
ilivyo katika injili yetu ya leo. Mamajusi siyo Waisraeli hivyo wanawakilisha watu
owte Mungu amejionyesha kwa watu wote hata sisi tuliopo hapa na kwa namna ya pekee
leo kupitia hawa zetu. Tumshukuru Mungu hata leo anaendelee kujionyesha kwetu. Mamajusi
waliona nyota ambayo kwayo Mungu aliwaelekeza kwenda kwa mtoto Yesu tunapenda kumwomba
mwenyewzi Mungu ili ninyi muwe nyota ya kuwaongoza watu kufika kwa Mungu. Ninyi mue
ile nyota ambapo watu watakapowaona katika maisha yenu ya kumcha Mungu waweze kutamani
kumpenda na kumtumikia yeye zidi ya vitu vingine vyote na wawafuate kama mamajusi
walivyofanya.
Maandiko ya Nabii Isaya 60, 1-6, yanadhihirisha wazi hilo watu
kutoka sehemu mbalimbali wakiwa na vitu mbalimbali wakienda kumtukuza Mungu. Katika
Isaya nusu mwanga utukufu wa Bwana wana na binti kutoka mbali utukufu wa habari na
utajiri wa mataifa misafara ya ngamia na watu kutoka Medina wakichukua dhahabu ubani
na manemane wakiutangaza ukuu wa Mungu. Hii ndiyo Epifania ya kweli.
Somo la
pili toka barua kwa Efe. 3,2-3,5-6 linazungumzia juu ya ufunuo wa siri ya Mungu ambayo
Mungu alidhamiria tangu awali. Ni mpango ambao makuhani wa kale waligusia lakini hawakujua
maana kamili ya mpango huo. Mpango huo ulikamilika tu kwa njia ya Yesu kristo. Katika
waraka kwa waefeso 1, 3-10, tunasoma juu ya wingi wa neema ya Mungu isiyopimika. Epifania
ufunuo wa Mungu kwa njia ya Kristo ndiyo maana kamili ya maandiko matakatifu.
Somo
la Injili tukumbuke kuwa ufunuo haukutokea kama hamu ya Mungu kujitosheleza bali kwa
ajili yetu Mungu anapenda kuwa hata sisi tuuone utukufu huo hivyo tuinuke tumwelekee
kama mamajusi walivyofanya. Yahitaji pia bidii yetu. Tujitoe sisi wenyewe kwake kama
zawadi asante kwa ………. Zetu ambao wametambua upendo huo wa Mungu. Hakika hatuna budi
kumshukuru Mungu siku hii ya leo pamoja na mtume Paulo kama anavyoandika katika waraka
kwa wakolosai 1:3,12-20 twamshukuru Mungu baba yake Bwana wetu Yesu Kristo siku zote
tukiwaombea mkishukuru Baba aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu
katika nuru…!
Matokeo ya ufunuo wake Bwana, tunawajibishwa ameweka wazi ushindi
na utukufu wake mbele ya dunia yote. Tumshukuru Mungu hata leo anaendelea kujionyesha
kwetu. Mamajusi waliona nyota ambayo kwayo Mungu aliwaekeleza kwenda kwa mtoto Yesu.
Tunapenda kumwomba mwenyezi Mungu ili ninyi muwe nyota ya kuwaongoza watu kufika kwa
Mungu. Ninyi muwe ile nyota ambapo watu watakapowaona katika maisha yenu ya kumcha
Mungu waweze kutamani kumpenda na kumtumikia yeye zaidi ya vitu vingine vyote na wawafuate
kama mamajusi walivyofanya.
1 Tim 6:14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa,
pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
2 Tim 4, 1-8 kwa
ufunuo wake kristo tunapata amri ya kuhubiri neno la Mungu ili upate taji la haki.
Tito
2,13 sisi tunatarajia baraka na mafunuo. Ebr 9:28 baada ya haya matarajio yetu ni
kushiriki utukufu wa Mungu aliyejifunua kwetu.
Sisi ndiyo ile nyota
sasa watu wakituona waweze kufika kwa yesu Ufunuo ni zawadi. Je sisi ni zawadi
au tutakuwa zawadi ya Mungu kwa wake? Ni bahati kukutana na Yesu uzima, je bahati
hiyo ipo pamoja nawe? Kutojali kutokuwa waangalifu kutofuatilia mambo ya maandiko
tutatumbukia katika harati kama Herode na wakuu na waandishi wa mwisho wake ni maangamizi
tumezoea walidhani wanajua kila kitu. Mwindishi mmoja anatuangalisha haitoshi tu
kuujua ukweli bali zaidi sana jinsi tulivyojiandaa kutembea na kuishi ukweli huo tulioufahamu
haitoshi tu kujua na pia kuishi kwa imani hivyo tulichokijua.
Imetayarishwa
na Pd. Reginald Mroso, C.PP.S. Siku kuu ya Epifania Januari 6, 2015