2015-01-03 12:33:52

Majadiliano ya kidini yajikite katika maisha ya kila siku!


Askofu Claude Rault wa Jimbo Katoliki la Laghouat Gardaia, nchini Algeria anasema, Kipindi cha Noeli kwa Wakristo na Siku kuu ya Maulidi kwa waamini wa dini ya Kiislam ni fursa muafaka kabisa wa kujenga na kuendeleza mchakato wa majadiliano ya kidini, ili kudumisha mshikamano wa upendo, haki na amani; mambo msingi yanayomwilishwa katika uhalisia wa maisha ya watu nchini Algeria.

Siku kuu hizi ziwe ni fursa ya kuendeleza upendo kwa Mungu na jirani, kwa kushikamana na kusaidiana kwa hali na mali, licha ya tofauti zao za kidini, kwani yote haya ni mambo yanayopaswa kuwaunganisha zaidi badala ya kuwajengea chuki na uhasama usiokuwa na mashiko, tija wala maendeleo kwa wanachi wa Algeria. Majadiliano ya kidini yanapaswa kusimikwa katika maisha ya kila siku, ili kujenga na kudumisha umoja, udugu na urafiki kati ya Wakristo na Waislam.

Upendo kwa Mungu na jirani kanuni msingi ambayo waamini wa dini hizi mbili wanapaswa kuizingatia na ikiwa kama wataimwilisha katika maisha yao ya kila siku, basi hapana shaka kwamba, amani inaweza kutawala na hivyo kusaidia katika mchakato wa maendeleo endelevu ya binadamu na ustawi wake.







All the contents on this site are copyrighted ©.