2015-01-02 09:29:18

Vumbi la Maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani


Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili ambayo imeadhimishwa hivi karibuni na Mama Kanisa, limekuwa ni tukio la pekee kabisa katika mwendelezo wa Maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani, uliotangazwa na Baba Mtakatifu Francisko. RealAudioMP3

Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume, limezindua mshikamano wa mnyororo wa sala, unaowataka Watawa wa ndani kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani kwa kuchangia kikamilifu katika sala, ili kuchachua maisha na utume wa watawa ndani ya Kanisa na jamii katika ujumla wake, kwa njia ya ushuhuda unaojikita katika: sala, tafakari, maisha ya kijumuiya na unabii.

Kwa upande wa Italia, Monasteri ya Mtakatifu Klara, iliyoko mjini Assisi ndiyo iliyokuwa ya kwanza kufungua mshikamano wa sala katika Maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani. Nchini Eritrea, monasteri iliyochagulia ni ile ya Bikira Maria Aliyepalizwa mbinguni, iliyoko Asmara.

Lengo ni kuhakikisha kwamba, Watawa wa ndani ambao wanajisadaka kwa ajili ya kusali na kutafakari Neno la Mungu, wanashiriki kikamilifu katika mchakato wa kuwaombea Watawa wanaotekeleza dhamana na utume wao sehemu mbali mbali za dunia, ili kwa moyo wa imani na ujasiri, waweze kweli kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika maisha yao.








All the contents on this site are copyrighted ©.