2014-12-22 09:37:36

Tambua, sasa Yesu yupo, anabisha hodi mlangoni mwa moyo wako


(Vatican Radio) Jumapili, Papa Francisko alitoa mwaliko kwa waamini na wengine wote, kusikiliza kwa makini sauti ya Mungu anayebisha hodi malangoni mwao. Papa alisema kwa mara nyingi , Yesu hupita katika maisha yetu, kutupatia ujumbe wa wokovu, lakini bahati mbaya sisi binadamu huwa tumezingirwa na mawazo mengi, na hivyo tunakosa nafasi ya kutafakari na kutambua taarifa ya malaika.

Baba Mtakatifu Francisko alitoa mwaliko huo wakati akizungumza na mahujaji waliokusanyika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kwa ajili ya Sala ya Malaika wa Bwana. Maelezo ya Papa, yalielekea katika yalijitokeza kwenye Liturujia ya Jumapili ya mwisho ya ujio, inayoeleza juu ya Malaika Mkuu Gabriel kumtokea Maria na kumtaarifu kuwa atapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na atamzaa masiye. Papa alieleza na kuonyesha kushangazwa na jinsi Maria alivyopokea ujumbe huu kwa unyenyekevu. Maria alisema "ndiyo". Alisema "Mimi ni mtumishi wa Bwana. Na ifanyike kwangu kama ulivyosema "(Luka 1, 38).


Papa Francis aliendelea kustajabia imani ya Maria ambaye hakujua kitakacho endelea , iwapo atapambana na uchungu mwingi au kuhatarisha maisha yake, lakini alishika jambo moja tu kwamba, Bwana amemtaka afanye jambo fulani , na yeye alilikubali kwa moyo mkunjufu, na matumaini makubwa. Maria alikuwa na imani kubwa! Papa alitaja kipengele kingine cha kuchukua kama kumbukumbu kwa Maria , ni uwezo wa Maria katika kuutambua “wakati wa Mungu". Katika tukio hili, alisema, Maria anatufundisha kutambua wakati mazuri ambamo Yesu hupita katika maisha yetu , akiomba tuwe tayari kutoa jibu la ukarimu.


Katika wakati huu wa Noeli, Papa aliendelea, Yesu anapita katika maisha yetu. Wakati wa Krismasi, Yesu yupo anabisha hodi katika moyo wa kila Mkristo na kila binadamu, akiitwa kujibu, kama Maria, kutoka jibu la kweli binafsi , kusema "ndiyo", na kujiweka wenyewe katika uwepo wa Mungu na huruma yake. Lakini Papa alionya , dhidi ya kukosa utambuzi huo, kutokana na hali ya kumezwa na mawazo kwa mambo ya kidunia, hata katika siku hizi za maandalizi ya Siku Kuu ya Krismasi. Kuna viashiria vingi lakini watu hawatambui kwamba, kama ni Bwana anayegonga hodi katika mioyo yetu, akisubiri kukaribishwa .

Baba Mtakatifu aliendelea kuonya umati dhidi ya watu kumezwa na mambo yao wenyewe , hata katika kipindi hiki cha maandalizi ya siku kuu ya Noeli. Kukosa hata utambuzi kwamba, ni wakati ambamo Bwana anagonga hodi katika milango ya mioyo, akiomba kukaribishwa ndani , akisubiri jibu la ndiyo.

Papa alirejea maneno ya Mtakatifu mmoja aliyesema , “Nina hofia kumkosa Bwana atakapo pita kwangu” Papa aliitaja hofu hii kuwa ni hofu ya kweli , yenye kutatambua uwepo wa Bwana, na hivyo kujiandaa kukutana naye na kutoa jibu, Ndiyo, na iwe kama ulivyosema. Ni hofu inayotakiwa kuwa katika kila moyo wa mtu, kusikiliza iwapo Bwana anagonga, subira yenye kumfanya mtu aboreshe maisha yake , kuwa karibu na watu wengine na Mungu.


Na Papa Francisko alihitimisha tafakari yake , akikumbuka unyenyekevu na ukimya wa Mtakatifu Yosefu na Maria kwamba, ni mwaliko kwa watu wote, kumkaribisha Yesu kwa uwazi; yeye anayekuja na kuleta zawadi ya amani: "amani duniani kwa wale ambao neema yake anakaa" ((Luka 2, 14). “Zawadi ya thamani ya Krismasi ni amani, imani yenyewe ni Kristo. Kristo anayegonga kwenye milango ya mioyo yetu kwa ajili ya kuijaza mioyo na amani yake. Fungueni milango kwa Kristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.