2014-12-22 15:42:06

Papa akutana na wasaidizi wake kutakiana heri za siku kuu ya Noeli


Jumatatu mapema , Papa Francisco, alikutana na wasaidizi wake, wakuu wa Idara na maofisa wa ngazi ya juu katika Ofisi za Curia ya Roma, katika ukumbi wa Mtakatifu Clementina, ndani ya Vatican, kwa lengo la kutakiana heri za Krismasi.

Akiwahutubia viongozi hao , alionyesha kufurahia jadi hii ya kukutana wakati wa mwisho wa kipindi cha majilio kwa ajili ya kutakiana heri, kwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana; tukio la Mungu aliyefanyika mwanadamu ili kuwaokoa watu, udhihirisho wa Mungu anayekuja kukaa kwetu, siri ya Mungu ambaye anachukua yeye mwenyewe, hali yetu ya kibinadamu na dhambi zetu, na kutufunulia maisha yake ya Kimungu, neema yake kubwa na msamaha wake wa bure. Papa aliendelea kueleza kwamba, ni yeye Yesu , aliyechaguliwa na Mungu, kuzaliwa katika hali ya umaskini ndani ya pango la Bethlehemu, kutufundisha nguvu ya unyenyekevu. Na hivyo kwa kweli, Krismasi pia ni sikukuu ya mwanga ambayo si tu kwa watu walioteuliwa, lakini kwa watu maskini, watu wa kawaida wanaosubiri wokovu wa Bwana."

Papa ameitumia nafasi hii kutoa shukurani zake za dhati kwa wakuu hao katika Curia ya Roma, wake kwa waume hasa kwa majitoleo yao ya kuhudumia Jimbo Takatifu na Kanisa Katoliki la Ulimwengu, na hasa Kiti Kitakatifu na Khalifa wa Mtume Petro. Papa pia aliwataja hata wale wanaostaafu kwa wakati na pia wale ambao Bwana amewaita nyumbani kwake , akisema wote wako katika mtima wa moyo wake. Na ameomba msamaha wa dhati kwa mapungufu yake , kimawazo, kimaneno na kimatendo.

Papa katika hotuba yake , iliyo angalisha katika Siku kuu ya Noeli, alilenga zaidi hasa wenye madaraka makubwa na mamlaka, kukumbuka kusitawisha roho wa huduma katika shughuli zao zote.

Aliasa kwamba, mara nyingi , viongozi hulemewa na kishawishi cha kujisikia wao ni mabwana wa wanyonge. Ni Mabwana kwa kila mtu na kila jambo, wakisahau kwamba, ni roho wa upendo, anayetakiwa kuhamasisha maisha yao ya huduma kwa kanisa la Ulimwengu , ni roho wa unyenyekevu na hasa katika mtazamo kwamba, hakuna mwenye mastahili au sifa za kuendelea kuishi milele katika dunia hii.

Papa ametaja majivuno kuwa ni ugonjwa mbaya wenye kuua. Roho huyo wa kujisikia ni bora au muhimu kuliko wengine ni kati ya maradhi mabaya ya dhambi kumi na tano. Papa alieleza na kutolea mfano wa roho ya Marta kwa Maria ,katika upangaji na ufanikishaji wa mipango, akisema, si kuvaa roho wa malalamiko daima, lakini wakati wa kuhudumia, wanapaswa kutenda siku zote bila malalamiko mengi.

Papa ametaja maradhi haya pamoja na matatizo mengine na majaribu mengine , huwa ni hatari kwa kila Mkristo na kwa yoyote aliye pewa dhamana ya kutawala iwe shirika, jumuiya, mabaraza, Parokia,au vyama vya kikanisa nk, huweza kujenga mgomo katika yote kama mtu binafsi au katika ngazi ya shirika.
Papa aliwakumbusha wakuu hao wa Idara kwamba, ni roho Mtakatifu peke yake, anayeweza kudumisha kila juhudi ya kweli katika utakaso na kila hamu halisi kwa ajili ya uongofu. Ni yeye huyo, anayewafanya kuelewa kwamba, kila mfanyakazi , anatakiwa kushiriki katika utakaso wa [fumbo] mwili Kristo, ambalo ni kanisa.

"Kwa hiyo, Papa aliwaambia, wakati huu wa kipindi cha Noel , na kama ilivyo katika muda wote wa mwaka mzima wameitwa katika kuhudumia, kwa mujibu wa ukweli wa Kazi kwa upendo, na kukua katika kila njia, katika yeye aliye kichwa, Yesu Kristo, kama mwili mzima wa Kanisa uliojengeka katika upendo.








All the contents on this site are copyrighted ©.