Mabalozi wapya wawasilisha hati zao za utambulisho!
Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 20 Desemba 2014 amepokea hati za utambulisho
kutoka kwa Balozi Jaime Bernardo anayeziwakilisha Nchi za Scandinavia mjini Vatican.
Baba Mtakatifu pia amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Clelio Galassi kutoka
Jamhuri ya Watu wa San Marino, moja ya nchi ndogo sana duniani.
Mwishoni,
Baba Mtakatifu Francisko amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Eduardo Fèlix
Valdes, anayeiwakilisha Argentina mjini Vatican. Itakumbukwa kwamba, Alhamisi, tarehe
19 Desemba 2014, Baba Mtakatifu alipokea hati za utambulisho kutoka kwa Mabalozi wapya
kumi na watu wanaoziwakilisha nchi zao mjini Vatican.