Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Katekesi yake kuhusu Familia, kwenye Uwanja wa
Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Jumatano tarehe 17 Desemba 2014, amewaalika
waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuwakumbuka na kusali kwa ajili ya watu waliofariki
dunia kutokana na vitendo vya kigaidi vilivyofanywa huko Sydney Australia na Pershawar,
nchini Pakistan.
Baba Mtakatifu anawaombea pumziko la milele wote waliofariki
katika matukio haya mawili pamoja na faraja kwa ndugu, jamaa na marafiki walioguswa
katika misiba hii. Anamwomba Mwenyezi Mungu aweze kuwaongoa na hatimaye kuachana na
matendo haya yanayoendelea kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao!