2014-12-13 10:39:18

Papa akutana na viongozi wa Jeshi la Wokovu


Baba Mtakatifu Francisco siku ya Ijumaa alikutana na viongozi wa Jeshi la Wokovu mjini Vatican. Katika hotuba yake , Papa alionyesha kufurahia na kutambua juhudi zao zinazojulikana katika kazi za uinjilishaji na huduma za kitume. Na kwamba ziara yao, ni matunda mazuri ya mawasiliano ya mara kwa mara katika miaka ya hivi karibuni, kati ya Jeshi la Wokovu na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Umoja wa Kikristo, ikiwa ni pamoja na mfululizo wa mazungumzo ya kiteolojia kwa lengo la kukuza uelewa mzuri kwa wengine, kuheshimiana na kushirikiana mara kwa mara.

Papa ameonyesha imani yake kwamba , Wakatoliki na Jeshi la Wokovu , wataweza kuendelea kutoa ushuhuda wao katika maisha ya kawaida kwa Kristo na Injili, katika ulimwengu wa sasa wenye kuwa na hitaji kubwa la kuiishi huruma ya Mungu isiyo kuwa na mipaka.

Papa aliendelea kusema, Wakatoliki na Jeshi la wokovu, kwa pamoja na Wakristo wengine, wanatambua kwamba wanahitaji wenye kuwa na kiu kwa Mungu, wana nafasi ya pekee katika moyo wa Mungu, kwa kuwa Bwana Yesu Kristo mwenyewe alikuwa maskini kwa ajili yetu (cf. 2 Kor 8: 9). Matokeo yake, Wakatoliki na Jeshi la Wokofu , mara nyingi hukutana katika maeneo ya pembezoni mwa jamii. Na hivyo yanakuwa ni matumaini ya Papa Francisco kwamba, imani ya pamoja katika Yesu Kristo Mwokozi, mpatanishi mmoja kati ya Mungu na mwanadamu (cf. 1 Tim 2: 5), inakuwa milele, msingi imara wa urafiki na ushirikiano kati ya Wakatoliki na Jeshi la Wokovu.

Aliendelea kusema, Kanisa ambalo hujitokeza mbele , ni jumuiya ya mitume wamisionari, wanaochukua hatua ya kwanza mbele , wale wanaojihusisha na kutoa mkono wa msaada , wenye kuzaa matunda na kufurahi. Ni jumuiya ya kueneza injili, inayotambua kwamba , ni mpango wa Bwana, ndiye aliyetupenda kwanza (cf. 1 Jn 4:19), na kwa hivyo tunaweza kusonga mbele, kwa ujasiri, kuchukua hatua, kuwaendea wengine, kuwatafuta wale waliokwisha kwenda mbali, kusimama katika njia panda, na kuwakaribisha wakiwa. Jumuiya kama hiyo ina hamu isiyokuwa na mwisho inayopenda kuionyesha huruma ya Mungu , na matunda ya uzoefu wake wa nguvu za Huruma ya Baba ya milele "(Waraka wa Kipapa wa Kitume wa Injili ya Furaha 24).

Baba Mtakatifu Francisco amewaambia viongozi wa Jeshi la Wokovu kwamba , anasali ili kwamba katika dunia ya leo, wafuasi wote wa Kristo waweze kutoa mchango wao katika kishawishi na nguvu sawia inayoonyeshwa na Jeshi la Wokovu katika utumishi wa kujitoa, wenye kupendwa sana. Pamoja na sifa hiyo, Papa aliendelea kutaja tofauti kati ya Wakatoliki na Jeshi la Wokovu kwamba ni hoja mbili za kiteolojia na kikanisa , tofauti hizo na visiwe vigezo vya kuzorotesha ushuhuda wa upendo wa Mungu wa pamoja na upendo kwa jirani, upendo ambayo una uweza wa kutoa msukumo kwa ahadi za pamoja ili kurejesha heshima ya wale ambao wanaishi pembezoni mwa jamii .

Papa Francisco alikamilisha hotuba yake na maneno kwamba , anatolea sala zake kwa Mungu kwa ajili ya kazi za Jeshi la Wokovu. Na watu wengine walio katika hali ngumu waendelee kutegemea juhudi za Jeshi la Wokovu , zinazoweza kuwaonyesha mwanga Kristo na kuangazia mahali pa giza katika wa maisha yao. Papa amelitakia Jeshi la Wokovu kujazwa na zawadi ya Roho Mtakatifu kwa hekima, ufahamu, ujasiri na amani, na hivyo kushuhudia Ufalme wa Bwana katika mateso ya dunia hii. Na kwamba anahitaji maombezi yao.








All the contents on this site are copyrighted ©.