2014-12-12 10:06:48

Ukatili ni vitendo vya kinyama, haviwezi kukubalika!


Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani linaungana na viongozi wa dini mbali mbali nchini humo kulaani mbinu za ukatili zilizotumiwa na Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, katika kupambana na watuhumiwa wa vitendo vya kigaidi. Askofu Oscar Cantù, Mwenyekiti wa Tume ya Masuala ya Kimataifa ya haki na amani anasema kwamba, Kanisa linaamini na kulaani vitendo vya ukatili kwa kuwa ni dhambi na kamwe, haviwezi kuhalalishwa kwa misingi yoyote ile.

Senate ya Marekani, hivi karibuni imepokea taarifa inayoonesha jinsi ambavyo CIA ilivyowanyanyasa na kuwatesa watu waliokuwa wanashutumiwa kwa vitendo vya kigaidi, mambo ambayo yanakwenda kinyume cha utu na haki msingi za binadamu. Senate ya Marekani inamtaka Rais wa nchi kuimarisha utawala wa sheria ili vitendo vya ukatili ambavyo vimeidhalilisha Marekani katika uso wa dunia visitokee tena.

Taarifa inaonesha kwamba, tangu yalipotokea mashambulizi ya kigaidi hapo tarehe 9 Novemba, Marekani imekuwa ikitumia ukatili mkubwa kwa watu waliokuwa wanashukiwa kuhusika na vitendo vya kigaidi.







All the contents on this site are copyrighted ©.