Kanisa ni mama anayetambua utajiri na mapungufu yake!
Furaha ya kanisa ni kuwa mama, kwenda kuwatafuta kondoo waliopotea. Papa Francisko
, alieleza Jumanne mapema wakati wa Ibada ya Misa, katika Kanisa la Mtakatifu Marta,
mjini Vatican. Alisema Kanisa haliwezi kuwa mhudumu kamilifu iwapo litakuwa na woga
na kujifungia na iwapo halitakuwa kama mama . Na hivyo , katika kuwa hivyo, mwaliko
unatolewa kwa Wakristo kuwa na furaha kwa ukombozi wa huruma wa Yesu
Baba Mtakatifu
Francisko, akilenga katika somo la kwanza ambamo Nabii Isaya anazungumzia dhiki
za wana wa Israel baada ya Uhamisho wa Babeli , homilia yake ilihimiza waamini kufungua
milango ya mioyo, kwa ukombozi wa Bwana. Watu - alisema – wana haja ya kufarijika
na ukombozi. Na uwepo wa Bwana hufariji. Faraja ambayo pia inaonekana wakati wa dhiki.
Lakini kwa bahati mbaya , Papa alionya, mara nyingi binadamu huikosa faraja hii kutokana
na uhaba wa imani, daima hutafuta faraja katika mambo yake mwenyewe. , hata katika
udhaifu wake na dhambi zake. Hiyo ndiyo asili ya ubinadamu wetu . Lakini kumbe ,
Papa alisisitiza , wakati Roho Mtakatifu anapokuja kutufariji , anatuletea hali nyingine
ambayo hatuwezi kuidhibiti, ila inakuwa ni hali halisi, ya kujiweka katika ukombozi
wa Bwana"
Na kwamba, faraja yenye nguvu zaidi ni huruma na msamaha. Papa
alieleza kwa kuangalisha mawazo katika mwisho wa sura ya kumi na sita ya Kitabu cha
Nabii Ezekiel, ambamo mnazungumzia orodha ya dhambi kwa watu wengi na kujisalimisha
na ulipizaji wa kisasi , faraja na msamaha Tafakari ya Papa iliendelea kutazama
ni ipi faraja inayopatikana katika kanisa. Na kwa jinsi gani na lini Kanisa hufurahi
apale mtu anapoisikia kufarijiwa na huruma ya Mungu na Msamaha wa Bwana , akisema
kuwa ni pale mtu anapoacha kujifungia ndani mwake mwenyewe.Ile furaha ya kutoka nje
kwenda kuwatafuta ndugu wengine wake kwa waume waliopotea , wale waliokwenda kwenda
mbali na kanisa .hiyo ndiyo furaha ya kanisa .Hapo Kanisa linakuwa kama Mama , linakuwa
kanisa hal lenye kuzaa matunda. Papa alieleza na kukemea tabia ya kanisa kujifungia
lenyewe, pengine kwa nia za kulinda taratibu zake au utendaji kamilifu, au katika
kutunza nafasi yake , kuwa safi , lakinikw kufanya hivyo hukosa furaha , hukusa sherehe
hukosa amani , na kuwa kanisa lisilo na imani, lenye wasiwasi na , huzuni, kanisa
ambayo ina zaidi ya mjane mgumba, kanisa kama hilo halihudumu lakini yanakuwa ni
makumbusho kanisa. Furaha ya Kanisa kuzaa matunda, furaha ya Kanisa ni kwenda nje
lenyewe kutoa maisha, furaha ya Kanisa ni kwenda kuangalia wale kondoo waliopotea,
furaha ya Kanisa ni hasa imo katika huruma ya mchungaji, huruma ya Mama Kanisa.
Mwisho
Papa alirejea tena kifungu kutoka Isaya, akielezea, kuyachukua maneno hayo , kama
mchungaji anayechunga kundi l wanakondoo wake kwa mikono yake mwenyewe . Hiyo ndiyo
furaha ya Kanisa kutoka nje ya lenyewe na kuzaa matunda. Papa alikamilisha kwa
kutolea sala akisema, "Bwana atupatie neema ya kazi, kuwa Wakristo wenye furaha katika
kuzalisha matunda, na aliomba ulinzi wa Mama Kanisa, uwalinde wana wake dhidi ya
kuanguka katika huzuni, hofu, tamaa na , wasiwasi nakatika kuwa kamilifu kwenye huduma
zake lakini hawana wazao. . Bwana utufariji na ukombozi wa mama kanisa utuwezeshe
kutoka nje ili wote wapate kufarijika na ukombozi wa huruma ya Yesu na huruma katika
msamaha wa dhambi zetu.