2014-12-06 16:06:46

Salam za rambi rambi kufuatia kifo cha Malkia Fabiola


Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambi rambi kwa Filippo, Mfalme wa Ubelgiji na wananchi wake, kufuatia kifo cha Malkia Fabiola, aliyefariki dunia Ijumaa, tarehe 5 Desemba 2014 akiwa na umri wa miaka 86. Baba Mtakatifu anaiombea roho ya Marehemu Malkia Fabiola, ipumzike kwa amani katika mwanga wa Ufalme wa Mungu.

Baba Mtakatifu anawahakikishia wale wote walioguswa na msiba huu, uwepo wake wa karibu kwa njia ya sala, ili waweze kuwa na matumaini katika maisha ya uzima wa milele.







All the contents on this site are copyrighted ©.