2014-12-03 14:40:50

Majadiliano ya kidini yanapania kujenga na kudumisha amani!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano asubuhi tarehe 3 Desemba 2014 amekutana na kuzungumza na viongozi wa dini ya Kiislam na Kikristo wanaofanya mkutano wao mjini Vatican chini ya uongozi wa Kardinali Jean Louis Tauran, Rais wa Baraza la Kipapa la Majadiliano ya kidini. Baba Mtakatifu amewashukuru na kuwapongeza kwa kumtembelea, jambo muhimu sana katika kukuza na kudumisha udugu kati ya watu!

Baba Mtakatifu anawapongeza kwa kazi na utume wao, katika mchakato unaopania kuwasaidia waamini wa dini hizi mbili kufahamiana vyema zaidi, ili kudumisha amani na utulivu. Baba Mtakatifu anasema, hii ndiyo njia ya amani inayojikita katika majadiliano ya kidini yanayosimikwa katika uhalisia wa maisha ya watu katika umoja, upendo na mshikamano wa dhati.







All the contents on this site are copyrighted ©.