2014-12-01 14:21:34

Balozi Pereira kutoka Costa Rica awasilisha hati za utambulisho kwa Papa Francisko


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe Mosi, Desemba 2014 amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Bwana Marco Vinicio Vargas Pereira, Balozi mpya wa Costa Rica mjini Vatican. Bwana Pereira alizaliwa tarehe 30 Agosti 1954. Baada ya masomo yake alijipatia shahada ya uzamivu kutoka Chuo kikuu cha Costa Rica na baadaye alijiendeleza katika masomo ya uhusiano na sheria za kimataifa.

Balozi Pereira amewahi kuwa mfanyakazi katika Wizara ya Mambo ya nchi za nje naushirikiano wa kimataifa kuanzia mwaka 1975 - 1978; Katibu mkuu wa Ubalozi wa Costa Rica nchini Brazil kuanzia mwaka 1979 hadi mwaka 1982. Baadaye kuanzia mwaka 1983 hadi mwaka 1989 aliteuliwa kuwa ni Mkuu wa Idara; Wizara ya Mambo ya nchi za nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kuanzia mwaka 1990 - 2003 alikuwa ni Mkurugenzi mkuu na Mshereheshaji mkuu wa taifa. Kunako mwaka 1992 hadi mwaka 1994 alikuwa ni mfanyakazi katika Ubalozi wa Costa Rica nchini Marekani.

Kati ya Mwaka 1998 hadi mwaka 2000 akateuliwa kuwa Balozi wa Costa Rica huko Belize. Kunako Mwaka 2003 hadi mwaka 2006 aliteuliwa kuwa Waziri mdogo wa mambo ya nchi za nje na kunako Mwaka 2006 hadi mwaka 2014 alikuwa ni Balozi wa Costa Rica nchini Uruguay.







All the contents on this site are copyrighted ©.