2014-11-30 10:25:27

Vitendo vya kigaidi Nigeria vinaendelea kusababisha maafa makubwa!


Rais Giorgio Napolitano wa Italia, amemwandikia ujumbe Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria kuonesha masikitiko yake kutokana na mauaji ya kinyama yaliyotokea Ijumaa huko Kano, Kaskazini mwa Nigeria na kusababisha watu zaidi ya 100 kupoteza maisha na wengine 135 kujeruhiwa vibaya, wakati walipokuwa wanasali kwenye Msikiti mkuu wa Kano.

Mauaji ya kinyama kutokana na misimamo mikali ya kidini ni jambo ambalo haliwezi kukubalika kuna haja kwa wananchi wa Nigeria kwa kushirikiana na Jumuiya ya Kimataifa kujifunga kibwebwe kupambana na vitendo hivi vya kigaidi. Rais Napolitano anapenda kutoa salam zake za rambi rambi kwa wote walioguswa na maafa haya na kwamba, wasikate tamaa kujenga na kuimarisha umoja wa kitaifa kama njia ya kupambana na vitendo vya kigaidi.

Vitendo vya kigaidi nchini Nigeria katika kipindi cha miaka sita nchini NIgeria vimepelekea uharibifu mkubwa wa nyumba za Ibada, shule, vituo vya Polisi, kambi za kijeshi na majengo ya Serikali. Rais Jonathan anasema wahusika watasakwa ili kufikishwa kwenye mkondo wa sheria!







All the contents on this site are copyrighted ©.