Rais Macky Sall wa Senegal akutana na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumanne, tarehe 18 Novemba 2014 amekutana na kuzungumza
na Rais Macky Sall wa Senegal ambaye baadaye amekutana na kuzungumza na Kardinali
Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique
Mamberti, aliyekuwa Katibu mkuu wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa
mjini Vatican.
Katika mazungumzo yao, viongozi hawa wawili wameridhika na mahusiano
mazuri yaliyoko kati ya pande hizi mbili pamoja na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa
na Kanisa katika sekta ya elimu, afya na katika mchakato wa majadiliano yanayopania
pamoja na mambo mengine kujenga na kudumisha umoja wa kitaifa. Baba Mtakatifu na mgeni
wake, wamegusia pia masuala ya kimataifa na kwa namna ya pekee, kinzani za kisiasa
zinazoendelea kujitokeza Afrika Magharibi.