Jumuiya ya wanafunzi Wakatoliki pamoja na Watanzania wanaoishi na kufanya kazi mjini
Roma, Jumapili tarehe 16 Novemba 2014, walikutana kusali kwa ajili ya kuomba baraka
na neema kwa Mwaka wa masomo 2014- 2015; kuombea amani na ustawi nchini Tanzania;
Kumkumbuka Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na kumwombea afya
njema Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania aliyefanyia operesheni hivi karibuni huko Marekani.
Ibada ya Misa
Takatifu ilifanyika kwenye Seminari kuu ya Wamissionari wa Damu Azizi ya Yesu, Kanda
ya Italia na kuhudhuria na umati mkubwa wa Mapadre, Watawa, Waseminari na Waamini
walei. Balozi James Msekela na Familia yake walihudhuria pia. Ibada ya Misa Takatifu
imeongozwa na Mheshimiwa Padre Alcuin Nyirenda, OSB aliyekazia umuhimu kwa waamini
ambao ni wajasiria mali kuchakarika ili kuhakikisha kwamba, wanatumia hekima katika
kupima na kutenda, ili wasije wakayakoroga, kuyakaanga au kuchemsha!