Jengeni utamaduni wa watu kukutana na wala si kupigana!
Baba Mtakatifu Francisko mara tu baada ya tafakari ya Sala ya Malaika a Bwana kwenye
Uwanja wa Kanisa kuu mjini Vatican, Jumapili tarehe 16 Novemba 2014, aliyaelekeza
mawazo yake mjini Roma ambako kwa siku za hivi karibuni kumekuwepo na mgogoro mkubwa
kati ya wahamiaji na wenyeji, mambo yanayojitokeza katika miji mbali mbali Barani
Ulaya, hasa katika maeneo yaliyoko pembezoni mwa miji; maeneo ambayo wakati mwingine
yamesahaulika, na hivyo kuwa ni chanzo kikuu cha migogoro ya kijamii.
Baba
Mtakatifu anawaalika viongozi katika ngazi mbali mbali kuhakikisha kwamba, wanajitahidi
kutafuta suluhu ya matatizo ya raia wao kabla mambo hayaharibika. Jumuiya za Kikristo
zisaidie kujenga na kudumisha mazingira ambayo yatawasaidia watu kukutana na wala
si kupigana. Wahamiaji na viongozi wa Serikali wanaweza kupata nafasi ya kuzungumza
kwa pamoja katika maeneo ya Parokia. Jambo la msingi ni kutoruhusu kamwe kinzani na
migongano ya kijamii ichukue nafasi ya majadiliano sanjari na kusikilizana kwa amani
na utulivu, ili kupanga kwa pamoja mambo msingi kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya
watu kwa kushirikishana!
Tarehe 16 Novemba 2014, ilikuwa ni Siku ya Kimataifa
kwa ajili ya kuwakumbuka watu waliokumbwa na ajali barabarani. Baba Mtakatifu Francisko
wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana amewakumbuka na kuwaombea watu walioathirika kutokan
ana ajali barabarani na kuwataka watu kuwa makini kwa kuheshimu sheria na kanuni za
usalama barabarani.