Rais wa Austria akutana na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 13 Novemba 2014 amekutana na kuzungumza
na Bwana Heinz Fischer, Rais wa Jamhuri ya Watu wa Austria ambaye baadaye alikutana
na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa amefuatana na Askofu
mkuu Dominique Mamberti, aliyekuwa Katibu mkuu wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano
wa kimataifa mjini Vatican.
Viongozi hawa katika mazungumzo yao, wameonesha
mahusiano mazuri yaliyopo kati ya pande hizi mbili pamoja na kujadili masuala ya kimataifa,
hususan umuhimu wa kudumisha uhuru wa kidini na haki msingi za binadamu; sanjari na
watu kujikita katika mchakato wa majadiliano ya kidini na kitamaduni. Mwishoni, viongozi
hawa wawili wamejadiliana kuhusu masuala tete ya kimataifa na hasa zaidi hali ilivyo
huko Mashariki ya Kati.