2014-11-13 10:24:22

Adhabu ya kifo!


Kufutwa au kuendelea kuwepo kwa adhabu ya kifo ni kati ya mada tete zinazojadiliwa na Bunge la Zimbabwe kwa wakati huu, kwani Zimbabwe ni kati ya nchi chache duniani ambazo zina adhabu ya kifo. Takwimu zinaonesha kwamba, tangu kunako mwaka 2004 adhabu ya kifo haijawahi kutekelezwa nchini Zimbabwe.

Bado kuna vuta ni kuvute ya kutaka kuendelea au kusitisha adhabu ya kifo inayoungwa mkono na Mwanasheria mkuu wa Zimbabwe Bwana Johanes Tomana, lakini anapingwa na Waziri wa sheria Bwana Emmerson Mnangagwa, moja ya wasaidizi wa karibu sana na Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe! Wachunguzi wa mambo wanasema, pengine Waziri huyu akamrithi Rais Mugabe!

Kanisa Katoliki linafundisha kwamba, maisha ya binadamu ni kitu kitakatifu kwani tangu mwanzo wake kinahusiana na kazi ya Mwenyezi Mungu ya kumuumba mwanadamu na hivyo kuwa na mahusiano ya pekee kabisa na binadamu, aliye peke yake kikomo chake. Mwenyezi Mungu peke yake ndiye asili ya uhai na hatima yake. Hakuna mazingira yoyote yanayoweza kujitwalia haki ya kuharibu moja kwa moja uhai wa binadamu. Watu wengi wanasema, adhabu ya kifo imepitwa na wakati.







All the contents on this site are copyrighted ©.