Rais wa Ghana akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 10 Novemba 2014 amekutana na kuzungumza
na Rais John Dramani Mahama wa Ghana pamoja na ujumbe wake, waliomtembelea mjini Vatican.
Rais Mahama baadaye amekutana na kuzungumza pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu
mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, aliyekuwa
Katibu mkuu wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.
Baba
Mtakatifu Francisko na mgeni wake katika mazungumzo yao, wamesifia mahusiano mazuri
yaliyopo kati ya pande hizi mbili sanjari na mchango wa Kanisa Katoliki katika ustawi
na maendeleo ya wananchi wa Ghana, hususan katika sekta ya elimu, afya pamoja na kuendeleza
mchakato wa majadiliano kati ya makundi mbali mbali nchini Ghana.
Viongozi
hawa kwa namna ya pekee, wamekazia umuhimu wa tunu msingi za maisha ya ndoa na familia.
Baadaye wamegusia pia masuala ya kimataifa na hasa kuhusiana na maafa makubwa ambayo
yamesababishwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, Afrika Magharibi.