Papa atembelea na kusali kwenye Makaburi ya watangulizi wake!
Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili jioni, tarehe 2 Novemba 2014, Siku ya kuwakumbuka
Marehemu Wote, jioni alitembelea na kusali kwenye makaburi ya watangulizi wake yaliyoko
chini ya Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican. Baba Mtakatifu alipata nafasi
ya kusali kwa kitambo kidogo mbele ya Kaburi la Mtakatifu Petro na baadaye aliwaongoza
waamini waliokuwepo huko kwa sala kwa ajili ya kuwakumbuka na kuwaombea Mapapa waliotangulia
mbele ya haki wakiwa na tumaini la ufufuko katika wafu na maisha ya uzima wa milele.
Ibada
ya Neno la Mungu imehuhuriwa na viongozi kadhaa kutoka Vatican, chini ya uongozi wa
Kardinali Angelo Comastri, kiongozi mkuu wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Mwishoni, Baba Mtakatifu Francisko alisali kwenye Makaburi ya Papa Yohane Paulo wa
kwanza, Mwenyeheri Paulo VI, Pio XII na Benedikto wa kumi na tano.