Jumuiya na vyama vya kiroho ni kazi ya Roho Mtakatifu - Papa
Ijumaa hii, Baba Mtakatifu Francisco amekutana na wajumbe kutoka jumuiya Katoliki
za udugu na usharika, ambao wako Roma kwa ajili ya Mkutano wao wa Kimataifa wa 16,
uliofunguliwa rasmi na Padre Raniero Cantalamesa, Mhubiri maarufu katika makazi ya
Papa. Hotuba ya Papa Francisco kwa wajumbe wa mkutano huo, amewaongoza washiriki
wa mkutano kutafakari kwa kina, maana ya kuwa na umoja katika utofauti.
Papa
amesema, Umoja haumaanishi usawa; wala haumaanishi kufanya kila kitu pamoja au kufikiri
katika njia hiyo hiyo moja. Umoja hauna mana ya mtu kupoteza utambulisho wake. Bali
Umoja katika utofauti ni kinyume na hayo, kwa kuwa ni kuitambua furaha ya kujumuika
na wengine na kuzikubali tofauti zao mbalimbali kuwa ni zawadi kutoka kwa Roho Mtakatifu,
anayo mjalia kila mmoja na ni kuweka ya zawadi hizo katika huduma ya wafuasi wote
wa Kanisa.
Umoja katika utofauti, Ina maana ya kujua jinsi ya kusikiliza
na kukubali tofauti, na kuwa na uhuru wa kufikiri tofauti na kujieleza mwenyewe kwa
heshima kamili, na kujongea wengine ambao ni kaka na dada zetu. Na hivyo hakuna sababu
za kuogopa au kuhofia tofauti! Papa alieleza na kurejea waraka wake wa Injili ya Furaha,
ambamo ametoa mfano wa tufe la dunia, ambalo hakuna upande unaozidi mwingine au kuwa
pakubwa kuliko pengine lakini pote umbali wake kutoka katikati ni sawia.
Papa
aliendelea kusema Kanisa linahitaji uvuvio wa Roho Mtakatifu , na kila Mkristu katika
maisha yake anahitaji kufunua moyo wake kwa utendaji Mtakatifu wa Roho Mtakatifu.
Roho iliyoahidiwa na Baba ambayo inamdhihirisha Yesu Kristo , anayetuongoza sisi kama
mtu binafsi kukutana Naye , na ambayo , katika kutenda kwake , huyabadilisha maisha.
Papa amewaambia wanajumuiya hao , iwapo uzoefu wanao katika masha yao, basi
wasiukalie, wanapashwa kuwashirikisha watu wengine, nao waweze kuwashirikisha wengine,
maisha ya Kiinjili na kuishuhudia.
Papa alifurahia madambiu waliochagua wka
ajili ya Mkutano huu: "Sifa na Ibada kwa ajili ya Uinjilishaji Mpya" . Papa alisema
Sifa ni "pumzi" ambayo inatupa maisha, kwa sababu ina uhusiano wa karibu na Mungu,
ni urafiki unaokua na kuimarika kupitia kumsifu Mungu kila siku. Kutoa sifa kwa Mungu
ni kuruhusu kupumua nje ya hewa hii ya maisha ya kiroho yenye kulishwa na sala na
maombi. Ni kupumua hewa inayomtangaza Yesu Kristo, katika muungano wa maisha kwa Roho
mmoja. Hakuna mtu anaweza kuishi bila kinga. Ni sawa kwa Mkristo: bila sala za masifu
na maombi, hakuna maisha ya Kikristo.
Papa amesema Karama hizi za kiroho ,
zinakumbusha Kanisa kwamba, uwepo wake ni wa lazima na muhimu kuwa na sala za kumsifu
Mungu. Na tunapo zungumzia maombi ya sifa katika Kanisa, mara akilini tunafikiri
juu ya jumuiya hizi za maombi na kusifu. Alieleza na kuhimiza kila Mkristo kuifunua
roho yake wazi ili Roho Mtakatifu aweze kutenda kazi yake na matunda yake yaweza
kuonekana nje katika kumsifu Mungu kwa sala na maombi na karama zingine kama nyimbo,
ngoma na muziki.