2014-10-30 08:33:57

Waandamana kupinga marekebisho ya Katiba!


Wananchi wa Burkina Faso, hivi karibuni wameandamana kupinga mabadiliko ya Katiba yanayotaka kumpatia nafasi Rais Blaise Campaorè kuendelea kubaki madarakani hata baada ya kumaliza muda wake wa kuongoza nchi kama Rais kwa awamu mbili kadiri ya Katiba ya nchi. Zaidi ya watu millioni moja walijimwaga barabarani na hapo wakakumbana na "mkono wa sheria", wakiwataka wanasiasa kuheshimu Katiba ya nchi ambayo kimsingi ni sheria mama.

Ikiwa kama Bunge litafanikiwa kurekebisha Katiba ya Nchi ya Burkina Faso, basi, Rais Campaorè atatinga tena kwenye kinyang'anyiro cha kuwania Urais kunako mwaka 2015. Itakumbukwa kwamba, aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi ya kijeshi kunako mwaka 1987, baada ya Rais Thomas Sankara kuuwawa kikatili. Kwa kipindi cha miaka kumi na minne ameongoza Serikali ya Burkina Faso.







All the contents on this site are copyrighted ©.