2014-10-27 10:56:58

Kura ya maoni kuhusiana na Muswada wa Katiba ni hapo tarehe 20 Aprili 2015


Serikali ya Tanzania umetangaza kwamba, tarehe 30 Aprili 2015, watanzania watapiga kura ya maoni kuhusiana na Muswada wa Katiba Mpya, kadiri ya tamko lililotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Tanzania Frederick Werema. Muswada wa sheria ambao umepitishwa hivi karibuni na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao maalum cha Bunge la Katiba, ndio utakaofanyiwa kazi siku hiyo.

Ikiwa kama Muswada wa Katiba Mpya utapitishwa, watanzania wanaweza kufanya uchaguzi mkuu kwa kutumia Katiba ambayo imekumbana na upinzani mkubwa kutoka ndani na nje ya Bunge maalum la Katiba, kiasi kwamba, baadhi ya wajumbe wakasusia kushiriki vikao vya Bunge.







All the contents on this site are copyrighted ©.