2014-10-22 10:42:33

Watu wa mataifa wanakutana mjini Vatican


Baraza la Kipapa la haki na amani kwa kushirikiana na Taasisi ya Kipapa ya Sayansi Jamii, kuanzia tarehe 27 hadi tarehe 29 Oktoba 2014 kwa pamoja wameandaa mkutano wa kimataifa kuhusu vyama vya watu kutoka sehemu mbali mbali duniani utakaofanyika mjini Roma.

Hivi ni vyama vinavyowawakilisha watu ambao wanaendelea kusukumizwa pembezoni mwa Jamii kutokana na utandawazi usiojali wala kuthamini utu na heshima ya heshima ya binadamu. Mkutano huu unatarajiwa kuhudhuriwa na wawakilishi wa watu wasiokuwa na fursa za ajira, wahamiaji na wale wanaojihusisha katika mchakato wa kuwajengea watu uwezo ili kukabiliana vyema na changamoto za maisha.

Kuna wawakilishi wa wakulima ambao wameng'olewa kutoka katika ardhi yao ili kuwapisha wenye nguvu kuwekeza katika sekta ya kilimo, makundi ya watu wanaoishi pembezoni mwa miji katika makazi yasiyokuwa rasmi kutokana na ukosefu wa makazi bora mijini. Baada ya mkutano huu, wajumbe wanatarajiwa kuanzisha mtandao wa kimataifa utakaosaidia kuratibu shughuli hizi kwa kusaidiana na Kanisa.







All the contents on this site are copyrighted ©.