Jumapili ijayo, Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI anatarajiwa kushiriki katika
Ibada ya Misa Takatifu mjini Vatican!
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI ni kati ya viongozi wakuu wa Kanisa wanaotarajiwa
kuhudhuria katika ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kumtangaza Mtumishi wa Mungu
Papa Paulo VI, Jumapili, tarehe 19 Oktoba 2014 majira ya asubuhi kwa saa za Ulaya.
Itakumbukwa kwamba, Baba Mtakatifu Benedikto XVI aliteuliwa na Papa Paulo VI kuwa
Kardinali.
Hadi sasa kuna Makardinali wawili ambao bado wako hai, hawa ni
wale walioteuliwa na Papa Paulo VI wakati alipokuwa analiongoza Kanisa. Hawa ni Kardinali
Evaristo Arns na Kardinali wakefield Baum. Haya yamesemwa na Padre Federico Lombardi
Msemaji mkuu wa Vatican, siku ya Ijumaa alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari
mjini Vatican.
Hili litakuwa ni tukio la pili la aina yake kwa Baba Mtakatifu
mstaafu Benedikto XVI kushiriki hadharani katika Ibada zinazoongozwa na Papa Francisko,
tangu alipong'atuka kutoka madarakani.