Wito na utume wa Familia katika Kanisa na Ulimwengu mamboleo! Kauli mbiu kwa Sinodi
ya Maaskofu kwa Mwaka 2015
Baba Mtakatifu Francisko ametangaza kwamba, maadhimisho ya awamu ya pili ya Sinodi
ya Maaskofu kuhusu familia yatafanyika kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 25 Oktoba 2015
mjini Vatican, yakiongozwa na kauli mbiu "Wito na Utume wa Familia katika Kanisa na
Ulimwengu mamboleo". Taarifa hii imetolewa na Kardinali Lorenzo Baldiseri, Jumatatu
tarehe 13 Oktoba 2014 wakati wa Kikao cha kumi na nne cha Sinodi maalum ya Maaskofu
kuhusu familia.
Mababa wa Sinodi wanaendelea na majadiliano kuhusu matatizo,
changamoto na fursa zilizopo katika familia, huku wakiongozwa na dhana ya ukweli,
uwazi na kwamba, Mababa wengi wa Sinodi wanaendelea kushirikisha uzoefu na mang'amuzi
yao kuhusiana na familia. Maadhimisho ya Sinodi, ambao ni muda maalum kwa Kanisa kutembea
kwa pamoja katika sala na tafakari yanahudhuriwa kwa sehemu kubwa na Baba Mtakatifu
Francisko.