Wananchi wana wasi wasi wa afya ya Rais Sata wa Zambia
Vyama vya kijamii nchini Zambia katika taarifa yake vinaonesha wasi wasi wao kuhusu
afya ya Rais Michael Sata baada ya kutoonekana hadharani kwa kipindi kirefu. hali
hii imepelekea vyombo vya habari vya kimataifa kuzungumzia kwamba, Rais Sata kwa sasa
anakabiliwa na hali tete ya afya. Rais Sata hivi karibuni alishindwa kuhutubia Bunge
la Zambia kutokana na sababu za kiafya, mambo ambayo yanaongeza wasi wasi kwa wananchi
wengi wa Zambia.
Wachunguzi wa mambo wanasema, tarehe 19 Septemba 2014, Rais
Sata alilazimika kufupisha hotuba yake na hivyo kuwaacha watu wengi wakiwa wameshikwa
na bumbuwazi. Hadi leo hii wananchi wa Zambia hawajapata majibu sahihi kuhusu afya
ya Rais Michael Sata. Vyama vya kiraia vinaliomba Bunge kuunda tume maalum ili kuchunguza
afya Rais Sata au vinginevyo, Rais aendelee kutekeleza wajibu wake barabara ili kuwahakikishia
wananchi wa Zambia kwamba, yuko "ngangari".