Baba Mtakatifu Francisko, anatarajiwa Jumamosi tarehe 18 Oktoba, majira ya mchana,
kukutana na kuzungumza na Waziri mkuu Nguyen Tan Dung wa Vietnam. Taarifa hii imetolewa
na Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican na kufafanua kwamba, hii itakuwa
ni fursa makini kwa Baba Mtakatifu pamoja na mgeni wake kufanya upembuzi yakinifu
kuhusu mahusiano kati ya Vietnam na Vatican.