2014-10-13 09:58:10

Mateka 27 wa Boko Haram waachiliwa huru nchini Cameroon


Rais Paul Biya wa Cameroon, mwishoni mwa juma ametangaza kwamba, Kikundi cha Boko Haram kimewaachia huru mateka ishirini na saba waliokuwa wametekwa hivi karibuni, Kaskazini mwa Cameroon. Watu hawa walitekwa nyara kunako tarehe 16 Mei huko Waza na tarehe 27 Julai huko Kolofata, maeneo ambayo yako Kaskazini mwa Cameroon na mpakani na Nigeria.

Wachunguzi wa mambo wanabainisha kwamba, pengine hata wale wanafunzi wasichana waliotekwa nyara huko Chibok, Nigeria wako katika eneo hili. Rais Biya akizungumza kwenye Radio ya taifa amefafanua kwamba, watu walioachaliwa huru wako salama, ingawa hakukupatikana ufafanuzi zaidi. Mateka hawa wameachiliwa huru wakati Jumuiya ya Kimataifa ikiendelea kushutumiwa kwa kutolivalia njuga tatizo la Boko Haram, wanaoendelea kuhatarisha amani na usalama Kaskazini mwa Afrika.







All the contents on this site are copyrighted ©.