2014-10-11 09:50:26

Kanisa Katoliki Kenya lakosoa kampeni ya chanjo ya pepopunda kwa wanawake


Tume ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya , ina mashaka na kampeni ya chanjo ya pepopunda inayolenga kutolewa kwa wanawake walio katika umri kati ya miaka 19-49, umri wa uzazi , ambayo itaanza wiki ijayo kama ilivyoandaliwa na Wizara ya Afya Kenya. Kanisa lina mashaka na mpango, ulioitwa kama ni mpango wa siri wa serikali, unaolenga kufanya wanawake wengi kuwa wagumba wanawake, kama hatua ya kudhibiti idadi ya watu.

Tamko hilo limenukuliwa na vyombo vya habari, kama lilivyotolewa na Tume ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya katika mkutano wa hivi karibuni uliofanyika katika Kituo cha Kichungaji cha Mtakatifu Patrick cha Kabula Bugoma . Tmko hilo lilitiwa sahihi Wenyekiti wa Tume Katoliki ya Afya Kenya, Askofu Paul Kariuki Njiru wa Embu na , Askofu Joseph Mbatia wa Nyahururu , kwa niaba ya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya . Tume hii ni pamoja na wasimamizi wa vituo 24 vya Afya vya majimbo Katoliki.

Tume imeilalamikia Wizara ya Afya, kuandaa kampeni hii ya chanjo kichinichini bila kuutangazia wazi umma sababu na athari za chanjo ya pepopunda. Na wametaka kujua kwa nini tangu mwanzo chanjo ya pepopunda haikuingizwa katika kampeni ya Shirika la Afya la Dunia WHO, chanjo dhidi ya polio na malaria.


"Tunataka kujua kama kuna mgogoro katika pepopunda Kenya, na kama ndivyo, kwa nini haikutangazwa waziwazi? Na kwa nini inalenga tu wanawake walio katika umri wa kuzaa, umri wa kati ya miaka 19-49; na kwa nini imewaacha nje wasichana wadogo, wavulana na wanaume iwapo wote wanaweza kukabiliwa na ugonjwa wa pepopunda? Na miongoni mwa magonjwa mengi yanayotishia maisha ya watu Kenya, kwa nini pepopunda imepewa kipaumbele? " Ni maswali yaliyoulizwa na viongozi wa kidini, walipokutana na waandishi wa habari katika Kituo cha Kichungaji cha Mtakatifu Patrick katika Kitongoji cha Kabula, Bungoma.


Naye Mkurugenzi wa huduma za tiba, Dr Nicholas Muraguri, akirejea upinzani huu amesema, hakuna sababu za kuwa na hofu juu ya chanjo ya pepopunda, i kwa kuwa ni kati ya chanjo msingi za kawaida, ambayo hutolewa kwa mama wajawazito wote nchini kote Kenya na kama ilivyo duniani kote. Na kwamba hawana tatizo na Kanisa na hivyo Mkuu wa kitengo cha Chanjo, Ephantus Maree anapanga kukutana na viongozi wa kanisa hivi karibuni, kuelezea umuhimu wa chanjo hiyo..

Pepopunda ni miongoni mwa magonjwa mengi ya kawaida, yenye kuwa na matokeo mabaya kwa wmama ya wanaojifungua hasa katika mazingira mchafu na wenye mazoea ya kufunga kitovu cha mtoto kwa kutumia njia asilia kama kufunga kwa kamba, na mzazi akipatwa na vijidudu vinavyo sababisha pepo punda anakuwa katika hatari ya kifo kwa asilimia 100 kama hakuwahi kutibiwa.


Dr Maree anasema , Kenya ni miongoni mwa nchi 28 duniani ambazo bado kutokomeza ugonjwa wa pepopunda, tangu WHO ianzishe kampeni yake mwaka 1989 kwa lengo la kufuta ugonjwa huo duniani ifikapo mwaka 1995. Kenya bado upo na hivyo serikali imeweka mkazo zaidi katika wilaya zake 60, hasa vitongoji 16 ambako ugonjwa pepopunda bado ni tishio la maisha.

Nalo Kanisa linasema, linataka serikali itoe taarifa za kutosha, ili umma kwa ujumla uelimishwe kwa lengo la kuepuka taarifa potofu na propaganda kuhusiana na chanjo hiyo, na heshima ya binadamu katika maisha na huduma za afya za lazima kama kipaumbele.








All the contents on this site are copyrighted ©.