2014-10-10 16:07:27

Papa: Mungu baba anatupatia zawadi kubwa ya Roho Mtakatifu:


Katika sala tunaomba mambo mengi lakini zawadi kubwa tunayoweza kupokea ni Roho Mtakatifu.
Ni maneno ya Papa Francisko katika Homilia yake Alhamisi 9 Okotaba katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatikan. Akitafakari juu ya Injli ya siku iliyokuwa ikimwonyesha mwanaume mmoja aliyekwenda usiku wa manane kwa rafiki yake ili apate kusikilizwa ombi lake.

Papa alisema, Mungu ana huruma, siyo kwamba anasamehe tu ,bali yeye ni mwema anatupatia zaidi ya kile tuombacho. Ni kwa sababu aliongeza, daima sisi tunaomba hiki na kile, na Mungu daima anatoa.

Alielendelea, katika Injili ilionyesha vitu vitatu, rafiki, baba na zawadi, kwa namna hiyo Yesu aliwaonyesha mitume namna ya kusali kupitia mfano wa mwanaume aliyekwenda usiku wa manane kwa rafiki yake kuomba chochote. Aliongeza kwamba, katika maisha kuna marafiki wema, ambao kiukweli hutoa kila kitu, lakini vilevile kuna hata wengine ambao ni wema hivihivi tu, kwa maana hata Biblia inasema kwamba, wapo wawili au watatu na siyo zaidi. Wengine ni marafiki lakini siyo kama hawa, maana wanatoa kadiri ulivyoomba.

Injili inaeleza, Papa aliongeza, kwamba Yesu aliweza kusema kwamba ni baba yupi kati yetu ambaye mtoto atomwomba samaki, na badala ya samaki apewe nyoka, au kuomba yai na apewa nge? Kama nyingi mliyo katili mnaweza kuwapatia kilichochema watoto wenu, ni jinsi gani Baba aliye mbinguni?

Aliendelea, siyo rafiki peke yake anayetusindikiza katika safari ya maisha, na kutupatia kile tunachokihitaji, bali yupo hata Baba wa mbinguni anayetupenda sana ambaye Yesu alisema kwamba anahangaikia hata ndege wa angani wapate chakula. Yesu anataka kuhamasisha imani katika sala, na anasema ombeni, mtapewa, tafuteni mtapewa, na bisheni mtafunguliwa kwahiyo Papa Francisco aliongeza, kuomba na kutafuta ni sawasawa na kubisha hodi katika moyo wa Mungu. Na Mungu atawapatia Roho Mtakatifu wote ambao wanaomuomba.

Hiyo ni zawadi kubwa ya Mungu, kwani Mungu hawezi kukupatia zawadi ambayo hukuomba vizuri na iwapo zawadi haina manufaa kwako. Lakini Bwana anatupatia zaidi Roho Mtakatifu, ambayo ndiyo zawadi ya kweli , na ambayo nafsi zetu hazijui kuomba.
Alimalizia Papa akisema sala lazima zinafanyika pamoja na rafiki, ambaye ndiye msindikizaji wa safari ya maisha,ifanyike kwa njia ya baba wa mbinguni na Roho Mtakatifu na rafiki Yesu.

Yesu anatusindikiza na anatufundisha kusali. Na sala yetu inapaswa kufanyika kwa njia ya Utatu Mtakatifu. Aliuliza kama wengine wanaamini, na kujibu ndiyo, na kama wanaamini Mungu, Je ni nani kwao?

Na kwa wengine wanaosema kuwa Mungu hayupo , aliwaonya kwamba wasikufuru kwa sababu Mungu yupo, Mungu Baba, mwana na Roho Mtakatifu yupo. Yesu anatusindikiza katika safari na kutupatia kile tuombacho;na Baba anatutunza na kutupenda, na pia kutuzawadia Roho Mtakatifu ambayo ni zawadi kubwa zaIdi.








All the contents on this site are copyrighted ©.