2014-10-09 09:06:05

Katekesi ya Papa : Wakristo kuweni na umoja...


Papa Francisco katika katekesi yake Jumatano 8Oktoba katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Vatikan, amegusia juu ya Wakristo wasiyokuwa Wakatoliki, akisema kwamba katekesi zilizopita alijaribu kuweka mwanga wa asili na uzuri wa Kanisa, na kujiuliza ni kitu gani kinafanya mtu awe mmojawapo wa watu wa Mungu ambao ni Kanisa.

Inabidi lakini tusisahau kwamba kuna wengine wanashiriki imani ya Kristo na Wakatoliki japokuwa siyo Wakatoliki bali ni wa madhehebu mengine, au wenye kuwa na kanuni tofauti na Wakatoliki.

Papa alibainisha kwamba wengi wamegawanyika na hata ndani ya Kanisa Katoliki,mgawanyiko huu unatokana na historia ya vurugu , mateso, na hata vita . Papa alisema hii ni aibu! Alikiri hata leo mahusiano siyo mazuri. Na kisha kuhoji, je sisi tunajiweka katika hali gani juu ya hilo jambo? Je na sisi tumejiachia au tunaamini kikamilifu kwamba tunapaswa kutembea pamoja kwenye mwelekeo wa mapatano na muungano kamili ? Ni muungano kamili wa kuweza kushiriki wote pamoja katika mwili na damu ya Yesu.
Mgawanyiko wa Wakristo, aliendelea , ukiumiza Kanisa, humumiza Kristo, pia na sisi tunapotengana tunamumiza Kristo: Kanisa kwa hakika ni mwili ambao Kristo ndiye Kiongozi. Papa alibainisha ; mnajua wazi ni jinsi gani umoja ulikuwa moyoni mwake Yesu kwa mitume wake alipowaeleza wabaki na umoja katika upendo wake. Inatosha tu kufikiria maneno yake kutoka Injili ya Mtakatifu Yohana, ambayo ni sala ikimwelekea Baba yake kabla ya mateso, na kusema “ Baba Mtakatifu, kwa jina lako ulionipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo (Yn 17,11)”.

Umoja huo ulikuwa tayari uko hatarini wakati Yesu yupo kati ya watu wake, aliendelea Papa kwamba, kwani katika Injili inaonyesha mitume wakijalidiliana ni nani atakuwa mkubwa kati yao. (cfr Lc 9,46)Bwana alikazia lakini juu ya umoja kwa jina lake Baba , akitaka watambue kwamba ushuhuda wao uwe wa ukweli ambao utaweza kuleta muungano na kutakiana mema, kwa hiyo mitume baadaye walitambua hadi Mtakatifu Paulo akafika na kuiambia Jumuiya wa Wakorinto kwa maneno haya: Basi ndugu nawasihi , kwa jina la Bwana wetu Yesu kristo , kwamba nyote mnene mamoja, wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja(1 Kor 1,10)”.

Papa aliongeza kwamba ni uchungu mwingi kwa mgawanyiko uliopo kati ya wakristo, tumegawanyika kati yetu, na wakati huo kuna jambo linalotuunganisha ambalo, wote tuaamni Yesu Kristo Bwana, wote tunaamini katika Baba , Mwana na Roho Mtakatifu na tatu wote tunatembea pamoja maana tupo safarini. Tunapaswa kusaidiana aliongeza Papa. Pamoja na kuwa katika jumuiya, kuna watu wenye akili, kuna wanatelojia wanaotafuta ukweli, kwa sababu ni lazima, lakini wote inabidi kutembea kwa pamoja.

Njia hii inayoitwa ya kiekumeni, ya kiroho ni kutembea njia ya maisha pamoja katika imani yetu ndani ya Bwana Yesu Kristo.
Katika Katekesi hii, Papa pia alikumbuka tukio lake mwenyewe la miaka 70 iliyopita, siku alipopokea kumunio ya kwanza, akieleza kwamba, kupata kumunio ya kwanza inabidi kila mmoja kutambua kuwa ni kufanya muungano wa ndugu wote wanao amini Yesu na wale wa kutoka madhehebu mengine.
Alimalizia Katekesi yake akisema, twende mbele tukitafuta ukamilifu wa umoja, pamoja na kwamba historia ilitutenganisha, lakini bado tupo safarini kuelekea mapatano na muungano. Huu ni kweli , na wote inabidi kutetea safari ya muungano. Tunapojisikia kukata tamaa na safari kuwa ndefu bila kufika , tukumbuke kwamba, Mungu hawezi kufunga masikio dhidi ya sauti ya Mwana wake Yesu anayesikiliza sala zetu ili Wakristo wote kweli wanakuwa kitu kimoja.








All the contents on this site are copyrighted ©.