Papa katika homilia yake, Jumanne 7Oktoba katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta
alitafakari somo la waraka wa Mtakatifu Paulo kwamba, Bwana alichagua watu wake
na kuwasindikiza kipindi chote cha maisha yao ya nyikani. Mtakatifu Paulo anakumbuka
maisha yake ya dhambi, na mambo ambayo Mungu aliyatenda kwa watu wake. Mtakatifu
Paulo hafichi dhambi zake , alizofanya yeye mwenyewe. Na hata sisi tunapaswa kukumbuka
kwamba tumetenda dhambi, alisema Papa.
"Sisi tulichaguliwa. Ni neema kubwa
ambayo tuliipata, ni neema ya upendo", Papa aliendelea kutafakari na kusema kufanya
kumbukumbu ni kuuona ukweli wa hali hiyo , kwani Paulo anaungama ni jinsi gani alivyo
vuruga Kanisa , na hasemi "mimi nilikuwa mwema , mimi nilikuwa mtoto wa yule, au
mwenye kuwa na uwezo", hapana , Paulo alisema "mimi nilikuwa mtesaji na mtu mbaya",
aliikumbuka safari yake ya maisha.
Papa alibainisha kwamba Kufanya kumbukumbu
ya namna hii katika maisha yetu kwa wengi ni nadra, wengi tunasahau mambo tunayoyaishi
muda huo huo, na si vyema kusahau ya nyuma, kama ilivyo kila mmoja wetu ana historia,
historia ya neema, historia ya dhambi, historia katika safari ya maisha, historia
ya mambo mengi. Papa alieleza na kuhimimiza kwamba, ni muhimu kusali kwa ajili ya
historia, Paulo alifanya hivyo akielezea kidogo historia yake na kwa ujumla anasema
kwamba Yeye alinichaguliwa, Yeye aliitwa, yeye aliokolewa, yeye alisindikizwa katika
safari ya maisha.
Kufanya kumbukumbu ya safari yako mwenyewe ni kutangaza utukufu
wa Mungu aliendelea Papa, kukumbuka dhambi zetu ambazo Bwana Mungu alituokoa,ni
kuupa utukufu wa Mungu. Mtakatifu Paulo anasema alimwokoa kwa mambo mawili dhambi
zake na neema ya Mungu msulibiwa.
Paulo alikuwa akifanya kumbukumbu yake
na kujisifu , nimekuwa mkosefu, lakini Kristo msulibiwa ameniokoa, na hivyo kufanya
kitendo hicho ilikuwa ni kujisifu, na hii ndiyo kumbukumbu ya Paulo ambayo hata sisi
tumeitwa kuifanya.
Aidha Papa alirejea somo la Injili ambamo Yesu anamwambia
Marta, unahangaika kwa mambo mengi , lakini kuna jambo moja tu, Maria amechagua nafasi
iliyo bora. Ni nini maana yake, Papa aliuliza, ni kumsikiliza Bwana na kufanyakumbukumbu,
haiwezekani kusali kila siku kama vile sisi hatuna historia, kila mmoja anayo ya
kwake, na katika historia hiyo ndiyo tunayo wakilisha katika sala kama alivyofanya
Maria. Lakini wakati mwingine tumejazwa mahangaiko kama ya Marta, kazi za kila siku
,katika kufanya kile ambacho tunapaswa kufanya, kinasasababisha kusahau historia
hii.
Uhusiano wetu na Mungu, Papa aliongeza hauanzi siku ya kubatizwa , unaaza
tangu Bwana alipotuangalia na kutuchagua , Ni katika moyo wa Mungu uhusiano unaanza,
wa kufanya kumbukumbu ya uchaguzi wetu ,ule unaotokana na utashi wa Mungu juu yetu.
Kumbukumbu ya safari yetu ya muungano. Je Muungano huo unaheshimiwa? Aliuliza.
Sisi
ni wadhambi na tunapaswa kufanya kumbukumbu , kufanya kumbumbu ya Mungu asiye katisha
tamaa,na yeye ndiye tumaini letu. Na hii ndiyo sala ya kweli Papa alimalizia homelia
yake akiwaomba wote kusali zaburi ya 138. E Bwana umenichunguza na kunijua. Wewe
wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;umelifahamu wazo langu tokea zamani ,Umepepeta
kwenda kwangu na kulaĆa kwangu. Hii ndiyo sala Papa alisema kusali ni kufanya
kumbukumbu mbele ya Mungu katika historia yetu, Kwa sababu historia yetu, ni historia
ya upendo juu yetu.