2014-10-05 16:10:04

Asilimia kubwa ya wazee duniani hawana pesheni !


Shirika la Kazi la Dunia ambao ni mkono wa Umoja wa Umoja wa Mataifa katika masuala yanayohusiana na kazi na ajira duniani, Jumatatu 30 Septemba, limeadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wazee Wastaafu na wito wa kutoa Kipaumbele katika utoaji wa “chanjo” ya pensheni na upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee .
Guy Ryder , Mkurugenzi Mkuu wa wa ILO, katika Siku hii ya Wazee, amesisitiza umuhimu wa kushughulikia masuala ya idadi ya watu kupitia sera jumuishi za kukuza ajira na ulinzi wa kijamii.
Tamko kutoka ILO linasema, maisha marefu na afya nzuri, ni moja ya matokeo muhimu zaidi katika maendeleo ya binadamu, katika kupimo cha uwezo wa binadamu katika kuboresha maisha ya binadamu, kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa sababu hii, ongezeko la kasi la idadi ya wazee katika nchi zote, zenye viwanda vingi na hata zile zenye viwanda vichache, tofauti katika kasi hiyo ni ndogo. Na kwamba kufikia mwaka 2050, inatarajiwa idadi ya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 65 itakuwa mara tatu zaidi, wakati idadi ya wenye kuwa na miaka chini ya 15 itabaki kama ilivyo au bila mabadiliko makubwa.
Na kwamba, Robo tatu ya watu wazima, watakuwa katika nchi katika nchi zenye viwanda vichache wengi wao wakiwa wanawake. ILO inasema, mabadiliko haya ya idadi ya watu, yatakuwa na athari kubwa pia katika mabadiliko ya dunia. Ni muhimu kuelewa hili, kama msaada kwa nchi kubadilisha sera zake juu ya maisha ya watu tangu sasa.

Ni maelezo ya Mkurugenzi wa ILO, Bwana Guy, akirejea repoti ya mwaka ya shirika lake. Anaendelea kusema, ili kukabiliana na changamoto hii, itakuwa muhimu kuwa na sera jumuishi zenye kuzingatia kukuza ajira na ulinzi wa kijamii na uwezo wa kuchochea mzunguko mzuri wa ajira, ulinzi wa kijamii na maendeleo. Baadhi ya nchi zimeonyesha kuwa macho juu ya sera za haki na ufanisi wa nafasi kwa ajili ya watu wazee. Ametaja sera hizo kuwa ni mchanganyiko wa sera, katika utambuzi wa umuhimu wa kutegemeana katika mabadiliko ya idadi ya watu, ajira, ulinzi wa kijamii, uhamiaji, kazi na maendeleo ya kiuchumi. Ni kukutana na changamoto za mazingira mpya ya idadi ya watu iliyoundwa na idadi ya watu wazee , majadiliano ya kijamii, yanakuwa ni muhimu kutambua majibu yanayo faa zaidi, kwa ajili ya ufanisi, usawa na ustawi endelevu.

Mkuu wa ILO, pia alitoa wito wa kuhakikisha wazee wanapata pensheni ya kutosha na huduma nzuri za afya, kama msingi umoja na mshikamano wa jamii, katika kuthamini utu wa mtu bila kujali umri. Kwa kutambua umuhimu wa usalama mapato katika umri wa mkubwa, katika nchi nyingi za kipato cha juu na pia katika baadhi ya mataifa yenye kipato cha kati, kipato cha pensheni kimepanuliwa vizuri kwa wazee. Lakini kwa nchi nyingi zenye kipato cha chini, malipo ya pensheni na huduma za afya kwa wastaafu na wazee kwa ujumla vipo katika hali za kusikitisha, hasa ikiathiriwa zaidi na ongezeko la kasi la Idadi ya watu.
Hivyo basi upanuzi wa pensheni, na upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee ni kipaumbele kwa ajili ya kila mtu. Adhimisho la mwaka huu la Siku ya Kimataifa ya wazee, ILO ilizindua ripoti “Hifadhi ya Jamii kwa Watu Wazee: mwenendo muhimu wa sera na takwimu”, ambayo ina uchambuzi wa kina juu ya mada hii ni muhimu sana hasa kwa wanawake wazee . Karibu nusu ya watu wazee katika ulimwengu hawana pensheni.
Kwa mujibu wa ripoti ILO, asilimia 52 ya wazee hupokea pensheni, lakini kwa viwango duni na hali imekuwa mbaya zaidi kama matokeo ya ukali wa kipeo cha uchumi duniani.









All the contents on this site are copyrighted ©.