Papa asema, binadamu ana tatizo la kumwekea Mungu masharti
Papa Francisko katika Homilia yake Ijumaa 3Octoba katika Kanisa dogo la Mtakatifu
Marta Vatican amesema kwamba ,hamu ya Mungu ni kukoa binadamu, lakini tatizo ni kwamba,
binadamu mara nyingi, hulazimisha sheria zake mwenyewe kwa wokovu wake.Ukaidi huo
wa binadamu umejitokeza katika maandishi mengi ya Biblia hadi kilele cha maisha ya
Kristo hapa duniani.
Papa Francisco alieleza hili kwa kuitafakari Injli ya
siku ambamo Yesu alionyesha huzuni juu ya watu wake walio mgeuzia kisogo kama neno
lake lisemalo “ kama Tiro na Sidoni wangepata miujiza ambayo imefanyika miongoni
mwenu, na Yesu kutoa onyo juu ya Korazin na Betsaida, kwa muda ule wangekuwa wameshaokoka.
Papa anaongeza kwamba, katika historia ya wokovu inaonyesha kama vile walivyowakataa
Manabii na kuwaua kabla yake, kwa sababu walionekana kubugudhi watu, na sasa walifanya
kitendo hicho kwa Yesu. Na hizi ni vurugu za upinzani dhidi ya waliokolewa zilizo
sababishwa na viongozi wa watu. Aliongeza.
Ni wale wale watawala wanaofunga
milango ambamo Mungu anapenda kuwaokoa. Na kwa namna hiyo walitambua mazungumzo
ya Yesu yenye nguvu kwa watawala wa nyakati hizo wanaopigana, na kumweka katika majaribu,
wanamwekea mtego kuona kama ataanguka, kwa sababu ni mpinzani dhidi ya waliokolewa.
Lakini Yesu anawaeleza kwamba yeye anawajua , maana wao ni kama vile watoto walio
pigiwa filimbi lakini hawakucheza,waliimbiwa maombolezo , lakini hawakulia, Je wanataka
nini? Papa alijibu kwamba wanataka kufanya njia zao za wokovu, kwamba hiyo ndi ndiyo
njia ya kumfungia Mungu milango.
Alimalizia akisema kwamba, Yeye anaamini kwamba
Yesu ni Mwalimu mwenye kufundisha njia ya wokovu.