UNHCR : fikirieni kwa makini umuhimu wa msaada kwa Wakimbizi
Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya wakimbizi , limetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa
kufikiria tena kwa makini, umuhimu wa ufadhili wa kibinadamu, mbele ya uso wa mtu
anayekimbia makazi yake kwa lengo la kusalimisha maisha yake yanayowekwa katika hatari
ya kuteketezwa bure. Ni ombi la AntoniĆ² Guterres Mkurugenzi Mkuu wa UNHCR, ambamo
amezungumzia mfumo wa kimataifa wa misaada ya kibinadamu, kwamba sasa uko katika
hatari ya kulemewa na mzigo wa migogoro mipya, Mashariki ya Kati na Afrika na usugu
wa migogoro ambayo bado kupata ufumbuzi huko Afghanistan, Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Congo, Somalia na Sudan na kwingineko.
Guterres alieleza hilo wakati
wa Mkutano wa Mwaka wa Kamati ya Tendaji ya Shirika la Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi
UNHCR, , ambamo aliieleza hali halisi ilivyo kwa upande wa ufadhili wa kifedha kwamba
kuongezeka kwa mahitaji ya kibinadamu, tayari, kimataifa kwa mwaka 2013 ilifikia
kuhitaji kiasi cha Dola za Marekani bilioni 22 , na kwa mwaka huu itakuwa zaidi ya
hapo kutokana na kasi ya ongezeko la mahitaji. Hii ina maana ya kufikiria katika
msingi ya fedha kwa ajili ya maendeleo na misaada ya kibinadamu.
Aliendelea
kusema mbali na mgogoro unaoendelea Syria, migogoro mpya ilipoanza katika Jamhuri
ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Ukraine na hivi karibuni Iraq, imesababisha mateso
ya kutisha na wimbi kubwa la wakimbizi na wahamiaji. Na kwamba Mashirika na Taasisi
kwa ajili ya kazi ya ubinadamu za Kimataifa, yaliyopewa dhamana ya kushughulikia
mahitaji haya, yanaona kila mgogoro mpya unaozuka huongeza kipeo cha ukosefu wa
mahitaji kutosha, katika utoaji wa misaada ya kibinadamu.
Kwa hali hiyo,
Mkurugenzi Mkuu wa UNHCR, Guterres, ameyaomba mataifa maskini yafanye kila linalowezekana
kuepusha shari za kivita na pale inapolazimu watu kukimbia ghasia, nchi jirani kwa
moyo wa ukarimu ziwe radhi kuwapokea wakimbizi na wahamiaji wa kulazimishwa. Pamoja
na wito huo amezishukuru serikali na wafadhili binafsi kwa msaada wao uliofanikisha
upatikanaji wa dola za Marekani bilioni 2.9 USD zilizotolewa kwa UNHCR na matawi
yake, kwa mwaka 2013. Na alitangaza hamu ya shirika lake katika , kuimarisha ushirikiano
na wabia wengine wa Umoja wa Mataifa na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na pia
kwa wale wanaohusika katika ushirikiano wa maendeleo. Anatumaini jumuiya ya kimataifa,
imeweza kujifunza vyema somo kutoka nchi za Mashariki ya Kati na migogoro mingine
inayo ongeza uhamiaji wa kulazimishwa, ikiwemo pia sababu kama vile ongezeko la
watu, ukuaji wa miji, umaskini na mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ni wazi inakuwa
ni kujibu swali juu ya utoshelevu na uendelevu wa rasilimali zilizopo, katika mahitaji
ya binadamu. Hata leo, pamoja kielelezo cha ongezeko la mahitaji , , mfumo wa fedha
katika misaada ya kibinadamu ni ukingoni mwa kushindwa.