Mkutano wa Mabalozi kutoka nchi za Mashariki ya Kati na Wakuu wa Curia ya Roma
Mabalozi katika nchi za Mashariki ya Kati kutoka Jimbo Takatifu, watakuwa na Mkutano
utakaoanza Alhamis 2-4Oktoba. Na washiriki wa mkutano huo ni Balozi nchini Misiri,
Yerusalem, Palestina, Jordan, Iraq , Iran , Libano, Siria , Uturuki, pia wawakilishi
wa kutoka Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York, na Gineva kwa upande wa Ulaya. Na
Vatican watakaohudhuria kikao hicho ni Makatibu wa idara za Curia ya Roma, Katibu
Mkuu wa Vatikan , Katibu msaidizi wa mahusiano ya nchi a nje , vilevile Kardinali
Fernando Filoni, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, ambaye alitumwa
na Baba Mtakatifu hivi karibuni kutembelea maeneo yaliyo na vurugu na ghasia za kivita
Mashariki ya Kati, pia wahusika wakuu katika Baraza la Kipapa hasa Usharika wa Makanisa
ya Mashariki ya kati, Baraza la Kipapa la Majadiliano ya kidini, na Baraza la kipapa
la haki na amani. Baba Mtakatifu Fransisco atasalimia wajumbe wa mkutano huu,
Alhamisi 2 Octoba wakati wa kufungua mkutano wao utakaomalizika Jumamosi 4Octoba asubuhi.