Siku ya Kimataifa ya Upashanaji Habari:Familia, nafasi ya upendeleo wa kukutana na
upendo
Mandhari ya Siku ya Kimataifa ya Upashanaji habari, kwa mwaka 2015 imetolewa chini
ya madambiu: “Kuwasiliana na familia: mazingira ya upendeleo wa kukutana na ufadhili
wa upendo". Mada iliyo chaguliwa na Papa Francisko ajili ya adhimisho hhilo la 49
ambalo litakuwa tarehe 17 Mei, 2015.
Taarifa inaeleza Papa Francisko amechagua
mada hii, kuwa mwendelezo wa madambiu ya mwaka jana na katika kuzingatia mazingira
ya sinodi mbili za Maaskofu juu ya familia, moja ikiwa mwaka huu na nyingine mwaka
kesho. Sinodi ambazo zinalenga kuwa na mchakato wa kina juu ya matatizo yanayokabili
familia leo hii na jinsi ya kukabilana na changamoto hizo, katika mtazamo wa kazi
za Kanisa za Kichungaji. Na hasa kwa kuzingatia kwamba, mara nyingi mabadiliko katika
utamaduni hayasaidii kuona jinsi ilivyo vyema kuwa na familia imara katika mfumo wa
jamii.
Ujumbe wa Papa kwa ajili ya siku hii ya Kimataifa ya Upashanaji Habari,
unalenga kuona jinsi uhusiano kati ya wanafamilia unavyovuviwa na kuongozwa na hulka
ya binadamu katika majitoleo kwa binadamu mwingine. Kwa kuheshimu na kukuza hadhi
ya mtu binafsi katika kila mmoja, kama msingi pekee wa thamani, majitoleo ya mtu
yanapata sura ya kukubalika, kukutana, mazungumzo, na huduma ya ukarimu na mshikamano
wa kina, kama Mtakatifu Papa Yohana Paulo II, alivyoandika katika waraka wake juu
ya Familia “Familiaris Consortio, N. 43) . Ujumbe huo unaendelea kutazamisha kwa
jinsi gani leo hii inawezekana kuwaambia watu hasa wale ambao wamepata kujeruhiwa
na kukatishwa tamaa kwamba upendo kati ya mwanaume na mwanamke ni jambo jema. Na kwa
jinsi gani inawezekana kusaidia watoto kujua kwamba wao ni zawadi yenye thamani kubwa
sana. Jinsi gani inawezekana kutia joto jipya mioyo ya watu, hasa wale ambao ni majeruhi
na walio kata tamaa, kuwasaidia kugundua upya uzuri wa upendo. Na kwa jinsi gani tunaweza
kuonyesha kwamba familia ni nafasi ya upendeleo ambamo mtu anaweza kuona uzuri wa
maisha, furaha na zawadi ya upendo, faraja ya msamaha inayotolewa na kupokelewa, na
kukutana na wengine.
Leo hii Kanisa lazima kujifunza tena, jinsi ya kuonyesha
kwamba, familia ni zawadi kubwa, ni kitu kizuri na cha thamani kubwa, na kwamba hilo
ndilo shina la jamii. Kwa hiyo basi, Kanisa linaitwa kuonyesha wazi zaidi kwamba,
zawadi ya upendo, ambayo bibi na bwana harusi huitoa kwa kati yao mmoja kwa mwingine,
inawavutia watu wote kwa Mungu. Papa Francisko ameeita ni kazi ya kusisimua, kwa
sababu ni hatua inayowaongoza watu katika kuutazama ukweli halisi wa binadamu, na
kufungua milango kwa siku zijazo, yaani, maisha.
Kanisa Katoliki duniani
kote, husherehekea Siku ya Kimataifa ya upashanaji Habari kwa mujibu wa Mtaguso Mkuu
wa pili Vatican, Kipengere("Inter Mirifica", 1963), kama yalivyo mapendekezo ya Maaskofu
wa Ulimwengu, ifanyike Jumapili kabla ya Pentekoste. Kwa mwaka ujao itakuwa Mei 17
2015. Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa ajili ya Siku Mawasiliano umechapishwa katika
jadi yake ya kuchapishwa kwa kushirikiana na Taaisisi ya Mtakatifu Francis de Sales,
msimamizi wa waandishi.