2014-09-19 15:25:53

Papa -Niombeeni kwa Mama wa Shauri Jema.


(Vatican Radio)Jumatano baada ya katekesi yake, Papa pia alizungumzia umuhimu wa ziara yake ya Kitume Albania Jumapili 21Septemba 2014 akisema kwamba; kwa msaada wa Mungu, ataweza kwenda Albania, kutembelea nchi hiyo sababu ya mateso makubwa waliyoyapata kutokana na utawala wa kidikiteta wa kikomunisti, na sasa hali ya amani imeanza kujionyesha katika ya madhehebu mbalimbali ya kidini.

Na aliwatumia salamu watu wa Albania akiwashukuru kwa maandalizi wanayo fanya kwa ajilli ya kumpokea. Na mwisho aliwaomba watu wote, wamsindikize kwa sala katika ziara hii. kuomba msaada wa Mama Maria wa shauri jema.

Katika matatizo yaliyowakumba watu wa huko Albania kwenye kipindi cha utawala wa kikomusiti Sista Maria Lucia wa Shirika la Mabinti Wadogo wa Yesu, anayefanya utume Tirana alipata ya kuongea na mwandishi wa habari wa Radio Vatican akisema inabidi kukumbuka kwamba Kanisa wakiwemo Wakatoliki Albania walipata masumbuko makubwa sana kwa kipindi cha utawala wa Enciver Hoxha.

Kwa kipindi cha miaka 50 wamekuwa kimya na Woga mkubwa, licha ya udikteita, utawala huo nchini Albania kulianguka miaka 23 iliyopita, na hivyo sehemu kubwa ya Mtaguso wa Pili wa Vatican unakosa katika kanisa katoliki la Albania.

La kushangaza baada ya kuanguka kwa utawala huo mwamko mzuri umekuwepo kwa watu wote wa Albania wakiwa wameungana na waislam,na Ortodosi katoliki .
Tangu mwanzo Kanisa la Albania limekuwa na uhusiano mzuri na wamisionari waliofika kwa mara ya kwanza kutoka nje, ni uhusiano ambao mpaka leo bado unaendelea ,pia miito kwa upande wa mapadre mahalia nao umeanza kuchanua, na zaidi kwa upande wa watawa wa kike na kiume, hii hakika ni ishara ya matumaini.

Pia sista alito ushuhuda wake kuhusu maelewano kati ya madhebu mbalimbali ya dini, kutokana na uzoefu wake alioufanya nchi ya Kosovo ambayo pia ilikuwa na hali kama hali ya nchi ya Albania, ya kwamba mwanzo walikuwa wakiishi katika vijiji vay pembeni na wakristo walikuwa wachache, zaidi walikuwa waislamu lakini pamoja na kuishi mchanayiko wa madhebu tofauti waliishi vizuri.

Katika mazingira ya mji mkuu Tirana anabainisha Sista kuna ushirikiano kati ya madhehebu yote ya kidini, waislam na wakatoliki na wanashiriki katika maisha ya furaha, kwa kupeana zawadi wakati wa sikukuu mbalimbali, wanapongezana na kusaidiana wakati wa shida.

Sista anamalizia akisema kwamba kitenda cha kufika Papa Fransisco katika nchi ya Albania ni muhimu sana , kwa kuwatia moyo wa kuendeleza ushirikiano na maelewano kati ya madhehebu, na zadi ya hayo katika harakati zinazofanyika kumpokea Papa anayo furaha kubwa kuona kuwa vyombo vya habari nchini Albania vimetoa kipaumbele juu ya ujio wa Papa Francisco.








All the contents on this site are copyrighted ©.