2014-09-13 08:41:41

UNCTAD yaadhimisha miaka 50


UNCTAD, chombo cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachoshughulikia masuala ya biashara na maendeleo, ni chombo muhimu katika masuala yote ya biashara, masoko, uwekezaji , mikopo, teknologia, wajasilimali na utoaji wa misaada ya maendeleo kwa ujumla. Chombo hiki (UNCTAD) kiliundwa mwaka 1964 kwa lengo la kusaidia maendeleo endelevu katika nchi zote zenye viwanda vichache duniani, nchi maskini.

Mikutano yake mikuu inapofanyika ni huzungumzia masuala ya biashara kwa ujumla na kutafuta muafaka pale inapojitokeza migogoro na utofauti wa maendeleo ya uchumi na pia kutokana na mabadiliko ya siasa.
15 - 26 Septemba 2014, unatarajiwa kufanyika Mkutano Mkuu wa Biashara na maendeleo huko Geneva Uswisi, sanjali na maadhimisho ya miaka 50 ya UNCTAD.
Kardinali Peter Turkson Rais wa Baraza la Kipapa katika uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa UNCTAD, anatarajia kutoa mchango wa Kanisa Katoliki katika shirika hili , kwa mujibu wa Mtaguso Mkuu wa pili wa Vatican .

Tangu mwanzo Baraza hili limekuwa na wasiwasi kutokana na kuongezeka kwa matatizo ambayo hata leo, sehemu kubwa ya watu wanazidi kuteseka. Mtaguso wa pili wa Vatican ulitaka chombo chake kuchochea Jumuiya katoliki kukuza maendeleo katika maeneo yao na jamii katika haki ya kimataifa.
"Mtakubaliana kila mtu kwamba maendeleo hayo ni lazima kusaidiana ili kuondokana na matatizo makubwa ya wanadamu, na maendeleo hayo yanapaswa kukuzwa".Ripoti inasema.
Miaka mitatu baada ya kuanzisha chombo, cha Umoja wa Mataifa UNCTAD 1964 kimejishughulisha na masuala ya maendeleo, hasa biashara ya kimataifa. Na Baraza kuu la kipapa walifanya mkutano na Papa Paulo wa IV , ambaye alitambua upeo wa mbali wa chombo hiki cha UNCTAD na kuona kuwa ni chombo bora kitakachoweza kufanya kazi daima na hasa pale kilipotoa tamko kuhusu“Maendeleo na jina jipya la amani”
Zaidi ya miaka 50 baadae, teknolojia mpya imevunja hali ya utamaduni na jadi katika mipaka ya mataifa na kufunguliwa kwa maeneo mapya na pia kukawepo fursa za kiuchumi. Aidha nguvu za uchumi zimepotea, na hasa kutokana na mapinduzi ya viwanda inayozidi kukua kwa haraka katika Asia ya Mashariki inayokwenda sambamba na mabadiliko ya utendaji mzima wa mfumo wa biashara ya kimataifa.
Lakini kuna swali la msingi ambalo bado linabaki yaani ni aina gani ya biashara na maendeleo inayotazamiwa kukutana na changamoto kama vile kuenea kwa umaskini na ukosefu wa usawa wa maendeleo?
Papa Paulo wa VI alifafanua ukweli na uwazi kamili wa maendeleo kwamba: “mendeleo ya kweli ni lazima kumwendeleza kila mtu kwa maneno mengine kila mtu binafsi (mwanamme, mwanamke na watoto)kila kundi la binadamu, na binadamu kwa ujumla .
Kwa nyakati zetu lakini, Papa Francis amesema kuwa"hadhi ya kila binadamu na kutekeleza azma ya manufaa ya wote ni wasiwasi unaodai kuboreshwa kwa sera za uchumi wote, kuliko kujaza hotuba za kisiasa katika mitazamo au mipango ya maendeleo “.
Uongozi wa kibinadamu au utawala bado unaonekana kuwa na mengi ya kujifunza kuhusu jinsi ya kuamuru masuala ya uchumi kwa ustawi wa kila mtu na kwa ulinzi wa mazingira.
Katika maneno ya Papa Francis: "Kwa heshima kutokana na kujitosheleza na utamaduni wa kila taifa, ni lazima kutokusahau kwamba dunia ni mali ya watu wote kwa maana ya watu wote; ukweli tu kwamba baadhi ya watu wanazaliwa katika maeneo yenye rasilimali chache au wako chini ya maendeleo,na hii haihalalishi wao kutothaminiwa au wakose heshima"
Ripoti ya Turkson inaeleza kwamba, dunia ni nzuri iwapo kuna utawala bora, umoja wa kimataifa, na haja ya kutambua uwepo wa walio bado katika hali za umaskini,wanaohitaji kuinuliwa. Mtakatifu Papa Yohane Paulo II alisema : umasikini siyo kama ni tatizo, lakini kama kama haja ya kuinuka nak utembea pamoja katika kuijenga dunia ya haki na usawa kwa kila binadamu kwa nyakti hizi na hata kwa siku za baadaye.

Anaongeza pia, Dunia yetu inautajiri tele, shukrani kwanza kwa ukarimu wa Muumbaji. Biasahara hakika ni ufunguo muhimu katika kuongoza maendeleo na itasaidia kukuza maendeleo halisi ya binadamu.








All the contents on this site are copyrighted ©.