Ahadi ya kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia na Vietnam
Papa Franciscko anafuatilia kwa karibu maendeleo katika mahusiano kati ya Jimbo Takatifu
na Nchi ya Vietnam na uhamasishaji wa Wakatoliki katika kuchangia maendeleo ya nchi
kwa manufaa ya wote na asasi za kiraia. Hilo lilielezwa Alhamis, baada ya kukamilika
kwa Kikao cha 5 cha Tume ya pamoja ya wajumbe kutoka Viet Nam – Jimbo Takatifu. Kikao
kilichofanyika mjini Hanoi Vietnam.
Taarifa inasema, kikao hiki cha siku
mbili mjini Hanoi, tarehe 10 na 11 Septemba 2014, kilifanyika kwa utulivu , maelewano
na urafiki, kama ambavyo ilvyokuwa katika vikae vyake vya awali,kikao cha mwisho kikiwa
Vatican Juni 2013 , chini ya mwenyekiti mwenza, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje
Vietnam, Mheshimiwa Bui Thanh aliyeongoza Ujumbe wa Vietnam, na Naibu Katibu wa Idara
ya Vatican kwa ajili ya mahusiano na nchi za kigeni, Askofu Antoine Camilleri, kama
mjumbe mwakilishi wa Jimbo la Papa.
Taarifa tokea kikao cha majuzi inaeleza
kwamba, Ujumbe wa Jimbo la Papa, ulionyesha kupendezwa na msaada unaotolewa katika
ngazi zote na Kanisa Katoliki nchini Vietnam katika utekelezaji utume wake. Na pia
uliweza kuona maendeleo yanayofanyika katika sera ya kidini Vietnam kama ilivyo jitokeza
mwaka 2013, haja ya kufanya marekebisho katika Katiba ya Vietnam, ili kwenda na nyakti
za utandawazi. Na hivyo marekebisho hayo yamewezesha mjumbe wa Jimbo la Papa, Mons.
Leopoldo Girelli kufanya ziara Vietnam. Ujumbe wa Jimbo la Papa umethibitisha hili
na kutaja kuwa ni hatua muhimu katika kuendeleza mahusiano na Vietnam na Asia kwa
ujumla, kama ilivyo jionyesha hivi karibuni wakati wa ziara ya Papa Asia.
Jimbo
Takatifu, linalenga kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na Vietnam na pamoja na Kanisa
Katoliki katika nchi hiyo , kuwa na fursa ya kuchangia kikamilifu zaidi katika maendeleo
ya nchi, hasa maeneo ya vijijini yanayoonekana kusahaulika ambako Kanisa Katoliki
pia liko.